Jokate Mwegelo akizungumza katika hafla hiyo
Jokate na Guoxun wakionyesha mikataba baada ya kusaini
Afisa Mtendaji mkuu wa kampuni ya Rainbow Shell Craft Company Limited (CEO), Deng Guoxun akuzungumza katika hafla hiyo
Wageni mbalimbali waalikwa wakishughudia hafla hiyo
Jokate akiteta jambo na Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa kwenye hafla hiyo
…………………………………………………………………………………………..
Na Mwandishi wetu
Dar
es Salaam. Mbunifu mavazi, Miss Tanzania wa namba mbili 2006,
mwanamuziki na muigizaji wa filamu, Jokate Mwegelo amesaini makubaliano
yenye thamani ya Sh8.5 billion na kampuni ya Kichina, Rainbow Shell
Craft Company Limited kwa ajili ya kuzalisha na kuuza bidhaa mbalimbali
za lebo yake ya Kidoti.
Makubaliano
hayo yalisainiwa jana kwenye hotel ya Serena baina ya Jokate na Afisa
Mtendaji mkuu wa kampuni ya Rainbow Shell Craft Company Limited (CEO),
Deng Guoxun.
Akizungumza
katika hafla hiyo, Jokate alisema kuwa makubaliano hayo ni ya kudumu
na kampuni hizo mbili zitazalisha na kuuza bidhaa za kidoti Tanzania
nzima na nje ya mipaka yake.
Alifafanua
kuwa kampuni ya China itawekeza Tanzania na kuwafaidisha watanzania kwa
kutoa nafasi ya ajira. Alisema kuwa pia wanatarajia kujenga kiwanda ili
kuinua uchumi wa nchi na maisha ya watanzania.
“Hii
ni hatua kubwa ya maendeleo kwangu, kama unavyojua, wakati naanza
kujishugulisha na masuala ya urembo, ubunifu na uanamitindo, sikutegemea
kufikia hatua hii ya kuingiza bidhaa zangu kimataifa, lakini sasa,
ndoto zangu zimetimia na najivunia mafanikio haya,” alisema Jokate.
Alisema
kuwa mbali ya kutoa mitindo tofauti ya kisasa ya nguo, kampuni yake pia
itazalisha aina mbali mbali za viatu, nywele ikiwa pamoja na mawigi,
weaving, Rasta na viatu vya wazi (sandals) ambazo kwa sasa zipo tayari
kwenye soko la Tanzania.
“Mpango
wangu ni kupanua soko la bidhaa zangu kama Kenya, Uganda, Burundi,
Rwanda, Afrika Kusini na nchi nyingine za Afrika,” alisema.
Afisa
Mtendaji wa Guoxun alisema kuwa wamefurahi kukamilisha ubia na kampuni
ya Kidoti na haya ni matunda ya ushirikiano wa kudumu baina ya serikali
yao na Tanzania.
“Tumefurahi
sana kukamilisha makubaliano haya, tunatarajia kuongoza katika soko la
hapa nchini na wenzetu (wachina) watafaidika pia, ” alisema Guoxun.
No comments:
Post a Comment