Mkurugenzi mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi huo.
BENKI ya CRDB imezindua kampeni maalum ya utumiaji wa huduma zake kupitia simu za mkononi 'SimBanking' kupitia kwa mawakala wa 'FahariHuduma'.
BENKI ya CRDB imezindua kampeni maalum ya utumiaji wa huduma zake kupitia simu za mkononi 'SimBanking' kupitia kwa mawakala wa 'FahariHuduma'.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa kampeni hiyo ijulikanayo kama
'Tuma Pesa na SimBanking Shinda Passo', Mkurugenzi Mtendaji wa Benki
hiyo, Dk. Charles Kimei alisema lengo la kuanzisha kampeni hiyo ni
kuwakumbusha wateja wake na watanzania wote kwa ujumla umuhimu wa
kutumia njia hizo mbadala ili kupata huduma kwa urahisi na uharaka.
Alisema
kampeni hiyo inatarajiwa kutoa magari kumi na mbili ambapo kila mwezi
mshindi mmoja atazawadiwa gari hilo, pamoja na zawadi ya gari la wateja
watakaotumia huduma hizo pia wataweza kujishindia zawadi nyingine
mbalimbali zikiwemo solar power, tables na simu za kisasa za mkononi.
"Tunataka
kuwavutia wateja wetu kuziamini na kuzitumia zaidi huduma hizi kwani ni
sawa kabisa na kupata huduma kupitia matawi yetu,".
Akielezea
namna ya kushiriki na jinsi mshindi atakavyopatikana, Dk. Kimei alisema
kuwa shindano hilo ni la wateja wote wa CRDB watumiao huduma hizo na
mshindi atakuwa ni yule mwenye miamala mingi zaidi kwa mwezi husika.
"Mshindi
ni yule atakayekuwa amefanya miamala mingi zaidi kwa kutumia SimBanking
au FahariHuduma katika mwezi husika, iwe ni kutumia fedha kwenda kwenye
akaunti nyingine, au kwenda kwenye mitandao ya simu au kulipia Ankara,"
alisema.
Kwa
upande wake ,Mwenyekiti Bodi ya Wakurugenzi CRDB, Martin Mmari alisema
ubunifu ndio njia pekee itakayotatua changamoto, ni muda muafaka kwa
Watanzania kuchangamkia fursa hiyo na kujishindia zawadi.
Mkurugenzi
wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa
akimkaribisha Mkurugenzi mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei
kuzungumza katika hafla ya uzinduzi wa kampeni maalumu ya utumiaji wa
huduma za benki hiyo kupitia simu za mkononi 'SimBanking', kupitia kwa
mawakala wa 'FahariHuduma', ijulikanayo kama 'Tuma pesa na SimBanking
shinda Passo' uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa (katikati) akiwa na maofisa wa benki hiyo.
Maofisa wa benki ya CRDB wakiwa katika uzinduzi huo.
Maofisa wa benki ya CRDB wakiwa katika uzinduzi huo.
Mwenyekiti
wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Martin Mmari, akikata utepe
wakati wa uzinduzi wa kampeni maalumu ya utumiaji wa huduma za benki
hiyo kupitia simu za mkononi 'SimBanking', kupitia kwa mawakala wa
'FahariHuduma', ijulikanayo kama 'Tuma pesa na simBanking shinda Passo'
No comments:
Post a Comment