ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Tuesday, January 8, 2013

Messi mchezaji bora wa dunia kwa mara ya nne



Messi akipokea tuzo yake
  
 Messi akishangilia moja ya mabao yake
 
 
Messi akishikilia kikombe cha ushindi
 
Messi akipongezwa na baadhi ya mashabiki

Mshambulizi wa Barcelona na timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi ameshinda tuzo ya Ballon d’Or kwa mwaka wa nne mfululizo. Messi, 25, alifunga jumla ya magoli 91 mwaka wa 2012 na aliwashinda wachezaji wengine Andres Iniesta wa Barcelona na Christiano Ronaldo wa Real Madrid.
Messi alikuwa miongoni mwa wachezaji watatu walioteuliwa na jopo la wandishi wa habari na makocha wa timu za taifa, manaodha wa timu hiyo wakiwa ni pamoja na Iniesta na Ronaldo.
Messi alitangazwa mshindi wa tuzo hiyo ya the Ballon d’Or, tuzo ambayo hukabithiwa mchezaji bora wa mwaka katika sherehe iliyofanyika mjini Zurich
Kwasasa Mesi ni mchezaji wa kwanza kuwahi kushinda tuzo hiyo ya Ballons d’Or, kwa miaka minne mfululizo, rekodi anayoshikilia na aliyekuwa mchezaji wa Ufaransa na rais wa UEFA kwa sasa Michel Platini.
Abby Wambach, alishinda tuzo kwa upande wa kina dada naye Vicente del Bosque, akituzwa kuwa kocha bora.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...