ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Wednesday, March 25, 2015

WIZARA YA NISHATI NA MADINI YATANGAZA UFADHILI WA MASOMO NCHINI CHINA KWA MWAKA 2015


 Msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Badra Masoud akizungumza na wanahabari.

  Msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Badra Masoud akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi, kuhusu ufadhili wa masomo nchini China kwa mwaka 2015. Kulia ni Ofisa Habari wa Maelezo, Fatma Salum.

 Mwanahabari Salome Kitomari kutoka gazeti la Nipashe, akiuliza maswali katika mkutano huo.

 Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.

Hapa mkutano ukiendelea.
Na Dotto Mwaibale
WIZARA ya Nishati na Madini imetangaza nafasi za masomo kwa vijana wa Tanzania kwa ufadhili wa Serikali ya Watu wa China kwa kipindi cha mwaka 2015.

Hayo yalibainishwa na Msemaji wa Wizara hiyo Badra Masoud Dar es Salaam leo wakati akizungumza na wanahabari.

Alisema nafasi hizo za masomo ni ngazi ya Shahada ya Juu ya Uzamili katika fani ya gesi katika Chuo Kikuu cha Jiosayansi cha China ambapo muda wa kutuma maombi hayo umeongezewa hadi kufikia Machi 30 mwaka huu.

Alisema waombaji wa ufadhili huo wanatakiwa kuwa na Shahada ya Sayansi ya Ardhi au Uhandisi kutoka vyuo vinavyotambuliwa na serikali, na muombaji awe na miaka kati ya 35 na 40.

Katika hatua nyingine Masoud alisema mitambo ya kuchakata gesi imekamilika kwa asilimia 96.

Alisema kukamilika kwa mitambo hiyo inamanufaa makubwa ikiwemo umeme wa uhakika na gharama nafuu kwani utekelezaji wa mradi huo utaliwezesha taifa kuokoa trilioni 1.6 kwa mwaka zinazotumika kununua mafuta kwa ajili yua kuzalisha umeme.

Masoud  alisema kukamilika kwa mradi huu kutachochea  maendeleo ya viwanda nchini kwani viwanda vingi vimeonyesha nia ya kutumia nishati  ya gesi asilimia  katika  kuendesha mitambo  yake  ya uzalishaji.aidha umeme wa uhakika utapunguza gharama za uzalishaji na kufanya  bidhaa za tanzania kukuzika katika masoko mbalimbali duniani.

Alisema tatizo la ajira nalo litapungua kutokana na kukamilika kwa mradi huu ambao utapelekea ajira  mpya  nyingi  kupatikana na kutokana na kuwepo kwa umeme wa kutosha na uhakika katika viwanda ambapo  viwanda  vingi vitaanzishwa vilevile umeme utakwenda mashambani na kwenye biashara nyingine hivyo kwa namna moja ama nyingine ajira  zitaongezeka. 

Alisema gesi hiyo asilia pia hutumika kama malighafi katika viwanda mbalimbali kama,mbolea, kemikali,aluminiamu pamoja na kutengeneza vifaa vya plastiki uanzishaji wa viwanda vipya kutokana na matumizi ya gesi  asilimia kutachochea 

kukua kwa uchumi  wa nchi yetu na kwa upatikanaji wa ajira mpya nyingi kwa vijana wetu. 

Aliongeza kuwa Serikali kupitia wizara hiyo chini ya Mradi Endelevu wa Usimamizi wa Rasilimali Madini (SMMRP), inakaribisha maombi ya Ruzuku Awamu ya pili kwa wachimbaji wadogo nchini. 

DIAMOND MOTORS WAZINDUA GARI JIPYA LA MITSUBISHI 2015 ASX JIJINI DAR


Wema Sepetu akiwasha gari Jipya la ASX Mitsubishi katika uzinduzi wa gari hilo jijini Dar es Salaam.

Hili ndilo gari la ASX Mitsubish jipya lililozinduliwa hivi karibuni katika hoteli ya serena jijini Dar es Salaam.(P.T)

Na Mwandishi wetu Dar es Salaam
Mtangazaji wa Clouds FM, Millard Ayo na mwigizaji maarufu nchini, Wema Sepetu wamesifia gari jipya la Mitsubishi ASX la mwaka 2015 linalouzwa na kusambazwa na kampuni ya Diamond Motors (Hansa Group).
Katika uzinduzi wa kutambulisha gari hilo uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, pamoja na mambo mengine Kampuni ya Diamond Motors wauzaji pekee wa magari kutoka Mitsubishi waliwaalika Millard Ayo na Wema Sepetu kujaribu gari hilo toleo jipya Mitsubishi ASX kabla ya uzinduzi. 
Mastaa hao walivutiwa na mwonekano wa Mitsubishi ASX lenye vioo vya kisasa juu vyenye mwanga unaomwezesha dereva na abiria kufurahia mwonekano wa pande zote.
Meneja mauzo wa Diamond Motors, Reena Ganatra alisema Gari hilo lenye luninga ndogo inayocheza DVD, iPods, Bluetooth na sauti kutoka vyanzo mbalimbali ni maalumu kwa vijana wa kisasa na familia kwani Mitsubish ASX limetengenezwa na teknolojia ya MIVEC yenye kulifanya liwe na nguvu ya 150 ps katika 6,000 rpm na nguvu ya kuzunguka kwa mwendokasi mkubwa na kwamba limetengenezwa maalum kutumia mafuta kidogo. 
“ASX ni mwanzo tu, tunazo aina nyingine za magari kama kama Pajero ambayo tunakaribia kuyatambulisha sokoni ili kuwapatia watanzania magari imara na yenye kuaminika kutoka Mitsubishi” Alisema Ganatra. 
ASX toleo la 2015 limebuniwa kwa ubora wa hali ya juu na imara likiwa na bodi gumu pia lina mfumo maalumu usiotegemea funguo hivyo kumfanya mwendeshaji kuwasha injini kwa kubofya kitufe.
“ASX kutoka Mitsubishi, imetengenezwa maalumu kukidhi mazingira ya Tanzania hasa mijini kama Dar es Salaam ambapo muda wowote dereva wa kawaida anatoka kwenye barabara nzuri na kuingia kwenye barabara zenye makorongo” alisema Ganatra
Injini ya gari hilo ambayo ni 2.0-liter imeunganishwa INVECS-III CVT inayoisaidia mwendelezo wake katika kubadili mwendo pamoja na uimara wa usukani unaosaidia mikono ya dereva kuwa salama hata anapokuwa katika mwendo mkali.
Hansa Group inayofanya biashara kama Diamond Motors Limited, imekuwa ikifanya kazi ya katika sekta ya usafirishaji tangu mwaka 1980, ikitoa huduma kwa wasambazaji na wadau wa usafiri.Kampuni hiyo huhusika na bidhaa/ huduma mbalimabali. Shughuli za Hansa Group zimesambaa karibu nchi zote za jumuia ya Africa ikitoa huduma kama vile za uchimbaji, Umeme, Mafuta na Gesi, Reli,Ulinzi, Ujenzi, Usafiri, kimataifa na jumuhia za kimataifa.

Mbaroni kwa viungo, mifupa ya albino

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Kagera, Henry Mwaibambe
 kamanda wa polisi mkoa wa kagere Henry mwaibambe
WATU wawili wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Kagera kwa kosa la kukutwa na viungo mbalimbali vya mwili ikiwemo mifupa mitatu ya mtu mwenye ulemavu wa ngozi (albino).
Kamanda wa Polisi mkoani Kagera Henry Mwaibambe alisema kuwa tukio hilo limetokea juzi katika kijiji cha Kyota kata ya Kimwani wilayani Muleba mkoani humo baada ya jeshi hilo kuweka mtego kwa watuhumiwa hao ambao walikuwa wanatafuta wateja wa viungo hivyo.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni James Rutozi (66) mkazi wa Kimwani ambaye ndiye aliyekuwa anahifadhi viungo hivyo na Emanueli Kaloli (50) ambaye pia ni mkazi wa Kimwani aliyekuwa anatafuta mteja wa viungo hivyo.
Alisema mara baada ya kupata taarifa kuwa kuna watu wanauza viungo hivyo kwa Sh milioni 3 waliweka pesa za mitego na kujifanya wao ni wateja na ndipo walipowakamata watuhumiwa hao wawili ambao walikutwa na mfupa mmoja na walipowabana zaidi ndipo walitoa mifupa miwili.
Alisema mnamo mwaka 2006 katika kijiji cha Rushwa kata ya Mushabago wilayani Muleba, Zeulia Jestus akiwa na miaka 24 mwenye ulemavu wa ngozi (albino) alifariki dunia muda mfupi baada ya kujifungua na ndipo watuhumiwa hao walifukua kaburi hilo mwaka 2008 kwa maelekezo ya mganga wa jadi.
Alisema pia walipotaka kujiridhisha jeshi hilo liliomba kibali mahakamani ili kufukua kaburi hilo mnamo Machi 23, mwaka huu lilipofukuliwa liligundulika kuwa viungo hivyo vimetolewa katika mwili wa marehemu huyo.
Aidha, jeshi hilo linamtafuta mganga wa jadi aitwaye Mutalemwa Revocatus ambaye ametoroka kabla hajakamatwa ambaye ndiye aliyewashawishi wafukue hilo kaburi na kuwapa dawa ya kinga ili wasidhurike wakati wanafukua.
Aliongeza kuwa mnamo mwaka 2008 wananchi wa kata hiyo ya Mushabago walitoa taarifa kwa Jeshi la Polisi kuwa kaburi alilozikwa marehemu Zeulia lilifukuliwa na watu wasiojulikana baada ya kugundua tukio hilo. 

CHANZO: HABARI LEO

Tahadhari: Wanamgambo wa Kislam wa ISIL Wanapanga Kuishambulia Tanzania



Kwa mujibu wa taarifa za kiupelelezi, Dola la kiislamu la ISIL, maarufu kama Islamic state. Linampango wa kujenga himaya yake Afrika mashariki, hasa Tanzania, Ethiopia, Kenya na Somalia. Hii ni kutaka kuungwa mkono na kujitanua zaidi kwenye nchi za Afrika. Pia Dola hilo limekuwa likipanga kuishashambulia Tanzania, hasa miji ya Mwanza na Dar Es Salaam.



Sakata la Urais, January Makamba Amlipua Lowassa,


January Makamba Amfungukia Lowassa.
 "Nafasi ya Urais ni nafasi ya hadhi na heshima kubwa. Unapoiomba hupaswi kufanya michezo ya kuigiza. Huu utaratibu wa kuratibu watu, kuwasafirisha, kuwapa posho na ubwabwa waje kukuomba kugombea ni michezo ya kuigiza ambayo ni aibu kubwa.
Kila mgombea ana uwezo wa kutengeneza WATU wa kumuomba kugombea lakini wengine hatufanyi hivi kwasababu tunaheshimu nafasi tunayoiomba na tunaamini kwamba haipaswi kutafutwa kwa ulaghai na maigizo.
Ni aibu sana kutumia shida na njaa za watu kisiasa. Ni aibu sana kukusanya vijana na wazee wa watu na kuwapangia viti na mahema na kuwapa pesa halafu pesa na kuwapiga picha. Ukiona mtu anatafuta nafasi ya uongozi kwa ujanja na ulaghai ujue atatawala kwa ujanja na ulaghai.
Viongozi wanaokubalika na watu hawangaiki kupanga Viti na mahema na kuwapiga picha watu wanaowakubali.

Mgombea anayehaha na kutumia pesa nyingi kuonyesha anakubalika ukweli ni kwamba hajiamini. Kama unakubalika huwezi kuratibu makundi na kuyalipa na kuwapiga picha na kuita waandishi wa habari waje kushuhudia. Hizo ni mbinu za mfa maji.

Naamini Chama changu hakitatishwa na nguvu za maigizo. Tunataka uongozi safi unaomuogopa mungu. Tunataka uongozi wenye uadilifu na fikra mpya za kuisogeza mbele Tanzania. Tunataka viongozi watakaomaliza shida za Watanzania sio wanaozitumia shida hizo kisiasa
Hata Mzee Makamba, pamoja na umri wake wa miaka 75, leo akiwa na pesa za kumwaga anaweza kutengeneza makundi yakamuombe kugombea Urais.

Ifike mahali katika nchi yetu tuache hii michezo. Tukiendelea na mambo haya, tunatengeneza taifa linaloendeshwa kwa propaganda tu. Watu wanaotaka kuomba nafasi ya Urais wanapaswa kuwa na ujasiri na wanapaswa kujiamini na kusema wanataka nafasi hiyo na wana fikra gani mpya bila kutumia pesa kuonyesha kwamba wanagombea kwasababu wanahitajika na watu. Uongozi thabiti na shupavu hautokani na michezo ya kuigiza."
January Makamba.

Tuesday, March 24, 2015

BONDIA MCHINA AWASILI Dar Es Salaam.

Rais wa oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO Yassini Abdalla kushoto akisalimiana na bondia Wang Xin Hua kutoka China mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Dar es salaam jana kwa ajili ya mpambano wake na mohamed Matumla utakaofanyika march 27 katika ukumbi wa diamond jubilee katikati ni Rais wa ngumi za kulipwa nchini PST Emanuel Mlundwa na kulia ni promota wa mpambano uho Jay Msangi.
Rais wa oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO Yassini Abdalla kushoto akisalimiana na bondia Wang Xin Hua kutoka China mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Dar es salaam jana kwa ajili ya mpambano wake na mohamed Matumla utakaofanyika march 27 katika ukumbi wa diamond jubilee katikati ni Rais wa ngumi za kulipwa nchini PST Emanuel Mlundwa.
bondia Wang Xin Hua kutoka China
Bondia Wang Xin Hua kutoka China akilakiwa na mwenyeji wake Rais wa ngumi za kulipwa nchini PST Emanuel Mlundwa

KINANA AWATAKA VIONGOZI WEZI, MAFISADI KUNG'OKA HARAKA CCM

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na msafara wake ukiwa umezingirwa na wananchi wa jamii ya kimasai ulipokuwa ukiondoka baada ya kuhutubia mkutano katika Kijiji cha Mtakuja, Kata ya Kia, Jimbo la Hai, mkoani Kilimanjaro leo, wakati wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua miradi inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM, pamoja na kusikiliza kero za Wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.

Komredi Kinana ambaye katika ziara yake ameambatana na Katibu wa Itikadiu na Uenezi, Nape Nnauye, ameutaka uongozi wa Kampuni ya Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro kuacha kuwabughudhi wananchi wa kata hiyo, baada ya kutoa mallamiko kuwa unataka kuwapora ardhi iliyo karibu na uwanja huo yenye ukubwa wa zaidi ya hekali 10,000 inayomilikiwa na vijiji 11.

Komredi Kinana amekemea tabia hiyo ya baadhi ya viongozi wanaopora kinguvu ardhi za wananchi. Pia amewahakikishia wananchi hao kuwa atasaidia kurejesha ardhi hiyo kwa kukutana na Rfais Jnakaya Kikwete na kumwambia juu ya dhulma hiyo/

Komredi Kinana , amesema kuwa kiongozi yeyote aliyeingia CCM kwa minajiri ya kutaka kujineneemesha binafsi kimaisha, kwanzia sasa hatakuwa na nafasi na inabidi aondoke katika chama hicho ambacho kazi yake ni kutetea haki za wanyonge.
 Komredi Kinana akishangiliwa na wananchi wa Kijiji hicho cha Mtakuja kinachokaliwa na jamii ya wamasai.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akishangiliwa na wananchi wa Kata ya Kia katika mkutano uliofanyika katika Kijiji cha Mtakuja.

 Wananchi wakishangilia baada ya kufurahishwa na hotuba ya Komredi Kinana.
 Wananchi wa Kata ya Kia, wakimpatia zawadi ya vazi la Kimasai pamoja na fimbo, Komredi Kinana wakati wa mkutano huo.
 Komredi Kinana akihutubia katika mkutao wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Mtakuja, Kata ya Kia, Jimbo la Hai, mkoani Kilimanjaro.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akihutubia mkutano wa hadhara mjini Hai leo. Jimbo hilo linaongozwa na Mbynge, Freeman Mbowe wa Chadema. Amesema mbunge huyo ajiandae kuachia jimbo hilo kwani katika uchaguzi wa mwezi Oktoba CCM mwaka huu itashinda kwa kishindo na kutwaa jimbo hilo
 Wananchi wakisikiliza kwa makini hotuba ya Komredi Kinana mjini Hai wakati wa mkutano wa hadhara.
 Waziri wa Elimu wa zamani, ambaye pia alikuwa waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Israel Nawinga, akimueleza jambo Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alipotembelewa na viongozi wa CCM kumjulia hali nyumbani kwake Losaa, Masama wilayani Hai leo.
 Komredi Kinana akishiriki kuchimba msingi wakati wa ujenzi mpya wa majengo ya Shule ya Msingi Modio iliyopatwa na jangoa la tetemeko na kubomoka eneo la Masama Mashariki, wilayani Hai.
 Watoto wanaosoma Shule ya Awali wakipita bila woga kwenye Daraja la zamani sana la Mnepo liliotengenezwa kwa kamba za waya katika Kijiji cha Kiyungi, wilayani Hai.
 Mmiliki wa Blogu hii, Kamanda Richard Mwaikenda akipita kwa uangalifu kwenye Daraja la zamani la Mnepo, wilayani Hai, Kilimanjaro leo.
 Komredi Kinana akishiriki kupaka rangialiposhiriki ujunzi wa daraja jipya la Mnepo lililojengwa kwa fedha za Serikali takribani sh. bilioni 1 katika Kijiji cha Kiyungi mpakani mwa wilaya za Hai na Moshi Vijijini.
 Komredi Kinana akikagua ujenzi wa Daraja jipya la Mnepo
 Komredi Kinana akipita kwenye daraja la zamani la Mnepo lililojengwa enzi za ukoloni katika Kijiji cha Kiyungi, mpakani mwa Wilaya za Hai na Moshi Vijijini. Daraja hilo limejengwa na kwa waya.
 Komredi Kinana akimkabidhi ng'ombe iliyotolewa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kwa Kijiji cha Kwasadala kilichofanya vizuri katika uchaguzi uliopita hivyo kuipatia CCM ushindi mnono. Pia kijiji hicho kilikabidhiwa gunia moja la mchele.
 Komredi Kinana akihutubia katika mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM Jimbo la Hai.
 Wananchi wakipiga picha za kumbukumbu wakati Komredi Kinana akihutubia katika Kijiji cha Mtakuja, Kata ya Kia, wilayani Hai.
 Komredi Kinana akizungumza na watumishi wa Hospitali ya Wilaya ya Hai, ambapo pia alikagua ujenzi wa chumba kipya cha Xray, katika Mji wa Bomang'ombe, wilayani Hai.
 Komredi Kinana akiijaribu mitambo ya Xray iliyopo katika chumba hicho cha upimaji kwa njia ya mionzi.
 Nape akipigwa mionzi (Xray) ya mkono wake wa kulia
Wauguzi na watumishi wa hospitali ya Wilaya ya Hai, wakiwa katika picha ya pamoja na Komredi
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...