ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Wednesday, February 19, 2014

Hii ndio Rekodi iliyowekwa na Rivaldo kucheza Timu moja na Mwanae


article-2562813-0052F7E400000258-867_634x451 
Mshindi wa kombe la dunia na mchezaji bora wa dunia wa zamani mbrazil Rivaldo ametengeneza historia mpya katika soka.
Mshambuliaji wa zamani wa FC Barcelona ameweka historia ya kucheza pamoja na mwanae wa kiume katika timu moja ndani ya uwanja ambao umepewa jina lake huko nchini Brazil. 
Rivaldo, 41, aliingia kama mbadala kwa timu ya Mogi Mirim wakati walipotoka sare ya 1-1 dhidi ya timu ya XV de Piracicaba katika ligi ya mji wa  Sao Paolo.
article-2562813-1BA1565700000578-863_634x611-1 
Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa baba na mtoto kucheza pamoja tangu Rivaldo mkubwa aliporejea nyumbani Brazil akitokea nchini Angola alipokuwa anaichezea klab ya Kabuscorp.
Mtoto wa Rivaldo ana miaka 18, ana kazi kubwa ya kufuata nyayo za baba yake na kuhakikisha anafika alipofika mzazi wake.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...