ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Friday, July 26, 2013

Marekani yaunga mkono kupeleka brigedi maalumu DRC ( Force Intervention Brigade)


 Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Bw. John Kerry, akizungumza wakati wa mkutano wa Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa, uliokuwa ukijadili hali katika eneo la Maziwa Makuu na uungaji mkono Mpango Mpana wa Kisiasa wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano wa Maendeleo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Maziwa Makuu.
 Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akizungumza kwa niaba ya Serikali.
Taswira ya Ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ulivyokuwa siku ya Alhamisi wakati wa mkutano uliojadili hali katika eneo la Maziwa Makuu, mkutano huo ulihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon, Mwakilishi wake wa Maziwa Makuu Mary Robinson, Mawaziri kutoka nchi za Maziwa Makuu, SADC , Umoja wa Afrika, EU, na Mkuu wa Banki ya Dunia aliyeongea kwa njia ya Video kutokea Makao Makuu ya Banki hiyo jijini Washington.
----
 Imeandikwa na Mwandishi Maalum, Umoja wa Mataifa, NY — Wakati  hali ya usalama  ikiendelea kuwa tete Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,  kufuatia   kuibuka upya kwa  mapigano hivi karibuni. Marekani  imetamka bayana mbele ya Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa,  kwamba, inakaribisha na kuunga mkono upelekaji wa  Brigedi Maalum ( Force Intervention Brigade) pamoja na mamlaka iliyopewa kupitia Azimio namba 2098 la 2013.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...