ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Wednesday, March 26, 2014

Yaliyowakuta Moyes na Ferguson kutoka kwa mashabiki baada ya kufungwa na City


1014006_853962921296815_988478712_n 
Mashabiki wa Manchester United waliojawa hasira jana usiku walimgeuka kocha wao wa zamani  Sir Alex Ferguson baada ya kushuhudia timu yao ikiadhibiwa na mahasimu wao  Manchester City  katika uwanja wao wa nyumbani Old Trafford usiku wa jana.
Vijana wa Manuel Pellegrini waliwatandika United 3-0 kupitia magoli ya Yaya Toure na Eden Dzeko na kuzidi kuwaondolea vijana wa Moyes kupata hata nafasi ya kushiriki michuano ya ulaya msimu ujao.
Na mashabiki wa United wakaamua kuhamishia hasira zao kwa Ferguson, ambaye ndio aliyemteua Moyes kumrithi nafasi yake. 1619658_684160054980210_667635377_n

Ferguson ambaye alikuwa jukwaani akitazama mchezo alikuwa akitupiwa maneno ya kejeli kuhusu uamuzi wake wa kumkabidhi timu Moyes wakati Moyes alikuwa akitukanwa kabisa na mashabiki kadhaa waliokuwa wamekaa karibu yake.
Hali ilizidi kuwa tata baada ya mashabiki kutaka kulishusha bango liliopo katika jukwaa la Stretford End ambalo limeandikwa ujumbe unaosomeka ‘Chosen One’ huku kukiwa na picha ya Moyes – hata hivyo polisi wa kulinda amani uwanjani walifanikiwa kuzima jaribio la mashabiki kulishusha bango hilo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...