ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Tuesday, September 16, 2014

MVUA ZALETA KIZAAZAA JIJINI DAR, Wazungu watembea peku.


Wananchi wakipita kwenye dimbwi la maji maeneo ya Posta Mpya jijini Dar es Salaam jana asubuhi baada ya kujaa maji. 
Eneo hilo ambalo lipo mkabala na Benki ya Posta kwa muda mrefu zimekuwa likijaa maji kutokana na mitaro ya Barabara ya Azikiwe kuziba lakini wahusika ambao ni Halmashauri ya Manispaa Ilala inaonesha wameshindwa kulimaliza hivyo kuleta usumbufu kwa watu wanatumia barabara hiyo pamoja na magari.
Kijana akipita kwenye dimbwi hilo huku akisukuma tolori lake lenye madumu.





Maji yakiwa yameeneo katikaeneo hilo karibu na kituo cha kuuzia mafuta.
Kijana akipita kwenye dimbwi hilo mbele ya maegesho ya Tax katika eneo hilo.
Mwendesha baiskeli ya magurudumu matatu akipita eneo hilo.


Wazungu waamua kutembea peku

Licha ya kuwepo kwa madimbwi ya maji yaliyochanganyikana na maji taka kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam , raia hao wa kigeni ambao hawakufahamika wanatoka taifa gani walinaswa na kamera ya mtandao wa habari za jamii.com wakipita maeneo ya posta mpya jirani na jengo la IPS wakiwa pekupeku jambo ambalo ni hatari kwa afya zao. 

Hata hivyo haikuweza kufahamika mara moja walikokuwa wakienda.
Kwa miaka ya hivi karibuni kumekuwa na baadhi ya madhehebu kutoka nje ya nchi ambayo waumini wake hawavai viatu kutokana na imani zao.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...