ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI
Showing posts with label China. Show all posts
Showing posts with label China. Show all posts

Wednesday, September 11, 2013

Waziri Mkuu Mizengo Pinda Aongoza Ufunguzi Wa Maonesho ya Bidhaa Zinazozalishwa nchini China Jijini Dar es Salaam


 Waziri Mkuu Mizengo Pinda alijaribu jembe la kupandia nafaka wakati alipotembelea banda la kiwanda cha Qingyuan  Manchu Autonomous County cha nchini China wakati wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini humo yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.Wanaomtazama ni Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Abdallah Kigoda (kushoto)  na  Balozi wa China nchini LV Youqing (kulia).
Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Abdallah Kigoda (katikati) akiongea na viongozi kutoka nchini China leo wakati wa sherehe za ufunguzi wa maonyesho  ya bidhaa zinazozalishwa nchini  humo yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
 Waziri Mkuu Mizengo Pinda (wa pili kulia) akikata utepe leo kuashiria ufunguzi wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini  China yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo ya siku nne yanalengo la kutangaza bidhaa zinazozalishwa nchini humo ili viwanda na makampuni ya nchi hiyo waweze kufanya biashara na watanzania. Kulia kwa waziri mkuu ni Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Abdallah Kigoda na kushoto kwake ni Balozi wa China nchini LV Youqing.
 Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiangalia mfano wa nyumba zinazojengwa na kampuni ya Beijing New Building Material alipotembelea banda hilo wakati wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini China  yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Wapili kulia  ni Waziri wa Viwanda na Biashara Dk. Abdallah Kigoda na watatu kushoto ni Meneja Msaidizi Idara ya Biashara 

 Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiangalia malighafi zinazotumiwa na  kampuni ya  Beijing New Building Material kutengenezea nyumba alipotembelea banda hilo leo wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini China  yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Wa kwanza  kushoto ni Meneja Msaidizi Idara ya Biashara ya Kimataifa  wa Kampuni hiyo Alec Lu na wapili kulia ni Makamu Meneja Mkuu Fred Yu.
 Mfanyakazi wa kiwanda cha Changzhou Amec Group cha nchini China Yan Xing Long (kulia) akimueleza Waziri Mkuu Mizengo Pinda jinsi mashine ya kuchanganya kokoto iliyotengenezwa na  kiwanda hicho  inavyofanya kazi  wakati wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini humo yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Baadhi wa watu mbalimbali walioshiriki  ufunguzi wa maonyesho ya bidhaa zinazozalishwa nchini China  yanayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Maonyesho hayo ya siku nne ambayo yamefunguliwa jana yanalengo la kutangaza bidhaa zinazozalishwa nchini humo ili viwanda na makampuni ya nchi hiyo yaweze  kufanya biashara na watanzania.Picha na Anna Nkinda – Maelezo

Saturday, August 31, 2013

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe azungumza na Mabalozi kutoka nchi tano Wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya usalama nchini DRC


 Mhe. Membe akitoa shukrani kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupitia Mabalozi hao kwa kulaani mauaji ya Mwanajeshi wa Tanzania yaliyotokea huko Mashariki mwa DRC tarehe 28 Agosti, 2013 kwa kushambuliwa na kundi la Waasi la M23  wakati Kikosi cha Kulinda Amani cha  Umoja wa Mataifa (MONUSCO)kwa kushirikiana na Majeshi ya Serikali ya DRC na Force Intervention Brigade (FIB) wakilinda amani. Anayesikiliza kwa makini ni Mhe. Alfonso Lenhardt, Balozi wa Marekani hapa nchini.
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini ambao pia nchi zao ni Wanachama wa Kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (Permanent 5) kuhusu  hali inayoendelea Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Mhe. Membe pia aliwapa taarifa za kuitishwa kwa Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) utakaofanyika mjini Kampala, Uganda tarehe 5 Septemba, 2013 kuhusu DRC. Nchi tano wanachama wa Baraza la Kudumu la Usalama la Umoja wa Mataifa ni China, Marekani, Ufaransa, Uingereza na Urusi. Mkutano na Mabalozi hao umefanyika Wizarani tarehe 30 Agosti, 2013.
 Balozi wa China hapa nchini, Mhe. Lu Youqing (kushoto) akitafakari jambo wakati wa mazungumzo yao na Mhe. Membe (hayupo pichani). Wengine ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Celestine Mushy (kulia) na Afisa kutoka Ubalozi wa China.
Balozi wa Uingereza hapa nchini, Mhe. Diana Melrose (wa tatu kushoto) akiwa na Wajumbe kutoka Urusi, Ufaransa na Marekani wakati wa Mkutano wao na Mhe. Membe (hayupo pichani) kuhusu hali nchini DRC.Picha na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

Tuesday, August 20, 2013

Rais Uhuru Kenyatta atembelea China

kenyattachina_289ae.jpg
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta alikutana na rais wa China Xi Jinping Jumatatu katika ziara rasmi mjini Beijing, inayolenga kuimarisha mahusiano kati ya nchi zao mbili. Wachambuzi wa maswala ya kisiasa hata hivyo wanasema huenda pia rais Kenyatta anatafuta rafiki mwenye ushawishi mkubwa kudhoofisha kesi ya mahakama ya kimataifa – ICC dhidi yake.
P.T

Bw. Kenyatta alikaribishwa rasmi na kwa taaadhima kuu na mwenyeji wake rais Jinping akiwa pamoja na wafanya biashara wa Kenya. Ziara hiyo inalenga kujenga mahusiano ya kiuchumi na China na kutafutia bidhaa za Kenya soko nchini humo.
Rais huyo wa Kenya alielezea manufaa ya ushirika wa China na Kenya, akitaja maendeleo na uwekezaji ambao umeimarisha miundombinu nchini mwake hususan barabara.
Bw. Kenyatta alikwenda China baada ya kukutana na maafisa wa Russia mjini Moscow ambapo pia alishuhudia wanariadha wa Kenya wakishindana katika mbio za masafa marefu na kujishindia medali kadhaa za dhahabu.
China na Russia ni wanachama wa kudumu katika baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na ni maarufu kwa kutumia kura ya turufu kupinga miswada yoyote yenye utata wa kisiasa. Maafisa wa Kenya na wale wa Umoja wa Afrika wamekuwa wakiliomba baraza hilo la Umoja wa Mataifa kuiomba mahakama ya kimataifa ICC kurejesha nchini Kenya kesi za uhalifu wa kivita dhidi ya rais Kenyatta na wakenya wengine.
Mchambuzi wa maswala ya kisiasa kutoka chuo kikuu cha Nairobi Adams Oloo aliiambia Sauti ya Amerika kuwa ziara ya rais Kenyatta inatoa ujumbe wazi kuwa Kenya inatafuta washirika wenye nguvu na kwamba haitegemei msaada wake kutoka nchi za Magharibi pekee

Wednesday, June 19, 2013

Ghana yawafukuza Wachina zaidi ya 200



  
Sehemu ya wachina Ambao ni wachimbaji haramu wa Dhahabu waliokamatwa huko Ghana na kurudihwa China
Baadhi ya wachimbaji haramu baada ya kukamatwa na jeshi la Ghana 
  
Wachimbaji haramu wakijaribu kuwarushia risasi maofisa wa Serikali wa Ghana walipokuwa wakiwasaka
 
Wachimbaji haramu wa Kichina huko Ghana
 
Ugomvi kati ya wachimbaji haramu wa Kighana na kichina ni kawaida na kuuana mara kwa mara
 
Wachimbajiharamu wakiandaliwa tayari kusafirishwa kwao China
 
Wachimbaji haramu wakitiwa ngucuni baada ya kurudihwa China



Nchi ya Ghana imefanya msako mkali uliopelekea kukamatwa kwa raiya zaidi ya 200 wa Kichina waliokuwa  wakifanya biashara haramu ya kuchimba dhahabu.
Kukamatwa kwa raia hao wengi wa kichina kumekuwa gumzo kubwa ulimwenguni na hasa bara la Afrika ambalo limeshuhudia ongezeko kubwa sana la raia wa Kichina ambao wanafanya biashara yeyote hata zile ndogo ndogo ambazo wazawa walikuwa wakizifanya.
Hata hivyo serikaki ya China imesema kwamba kukamatwa kwa raia hao hakutaathiri uhusiana uliopo kati ya Ghana na China. China inaliona Bara la Afrika kama mhilili mkubwa kwa ajili ya mali ghafi za viwanda vyake na mafuta.
Xuejum Oiu afisa katika wizara ya mambo ya nje ya China alisema kuwa uhusiano wan chi hizo mbili utaendelea kuimarika pamoja na kuwepo kwa hali hiyo ya raia wake kufanya uhalifu wa namna niyo huko Ghana, kufuatia msafara wake ulioenda Ghana kukutana na Rais John Mahama kujaribu kumaliza tatizo hilo.
Maofisa wa Ghana walifanya msako mkali mwezi huu na kuwakamata Wachina 202 ambao walikuwa wakichimba madini bila vibali. Maofisa hao walishafanya msako kama huo mara kwa mara lakini haukuwa mkubwa hivi. Wachimba madini hao wengi wao ni kutoka Shan Lin huko Guangzi Zhang kusini mwa China ambamo serekali ya china haijawapa kimaumbele kama sehemu nyingine.
Msemaji wa Serikali wa Ghana amesema kuwa raia 218 walisharudishwa kwao na sasa hawataruhusiwa tena kuingia Ghana “prohibited immigrants”
Mamia ya raia wengine wa China wanatarajiwa kuondoka wenyewe kwa hiari, ingawa chanzo cha habari hakijafafanua ni kwanini.
Uongozi wa Ghana umesema kwamba ukamataji huo haukuwahusisha Wachina peke yao lakini msako huo unatokana na hofu kwamba taifa kubwa la kichina kwa kutumia uweza wake wa kifedha litaweza kumeza uchumi wa taifa la Ghana. Ghana ni kati ya mataifa machache ya Afrika linaloonyesha uchumi imara na uchumi unaokuwa kwa kasi kubwa sana.  Ghana hata hivyo ni ya pili kwa uchimbaji wa dhahabu kwa wingi duniani. Kampuni kubwa kabisa inayojulikana kama AgloGold Ashanti inayochimba katika eneo la  Obuasi likiwa eneo lenye dhahabu nyingi mno.
 Biashara kati ya Ghana na China inafikia dola za kimarekani 5.43 bilioni. Ufanyaji wa biashra haramu umeelezewa kuweza kuharibu uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi hizo mbili.
Ninaipongeza serikali ya Ghana kwa kuthubutu na kuweza kufanya ilichokifanya.  Hapa Tanzania, Wachina wamezagaa kila kona, wanafanya biashara nyingi ambazo hata huwezi kuamini kama  kweli wamepata kibali cha kufanya hivyo. Pamoja na kuwa na ufanisi katika shughuli zao, tukumbuke kwamba fursa za kibiashara za wazawa zinasibwa kwa kuwa ni vigumu kuwa na ushindani hata kama tuko kwenye soko husia. Sidhani kama  kituo cha uwekezaji kinakubali kumsajili mwekezaji wa kichina anayekuja kuuza mitumba, viatu………. Na kusamehewa kodi. Mimi ni mmoja wa wafanya biashara ambao waliwahi kusafiri  kwenda China na kufanya biashara. Kwa sasa nyingi ya biashara zile zimekuwa ngumu kwa kuwa wa Wachina wenyewe wamekuwa maajenti na wauzaji. Unienda kariakoo sasa utakuta Mtanzania anauza nguo, na mchina anauza nguo zile zile. Tofauti ni kwamba mchina ndiye mwenye kiwanda na muuzaji na hapo hapo anakuja kama mwekezaji hivyo ana unafuu Fulani wa kodi. Matkeo yake  Mtanzania atashindwa kwenye ushindani usio sawa wa kibiashara Mchina atanawiri. Vivyo hivyo kwenye magereji………………….
Tufike mahali tuweke uzalendo mbele, tulinde mali zetu na biashara za watu wetu. Majuzi tu wamekamatwa na udongo huko kanda ya ziwa (kimya) wengine unasikia wamekamatwa na pembe za ndovu (kimya) Siku si nyingi wataanza kuuza hadi karanga mitaani na kahawa za mia mia, sisi tumekaa tu kimya.
Ghana wametuonyesha mfano tuige mfano huo ili kulinda rasilimali zetu na biashara zetu kwa ustawi wa nchi yetu.

Thursday, May 30, 2013

Mtoto aokolewa kwenye bomba la choo huko China


Polisi na waokoaji wakikata bomba ili kumwokoa mtoto aliyeflashiwa chooni.
 Sehemu ya bomba ambapo mtoto huyo alikwama
 The tiny face of a newborn baby boy is revealed as rescuers cut apart a sewage pipe at a hospital in Jinhua, China, on Saturday, May 25.
Uso wa mtoto huyo ukionekana akiwa katika bomba la choo
Nurses attend to the infant inside a local hospital. 
Madaktari wakihangaika kuokoa maisha ya kichanga huyo
The newborn baby is pictured in the hospital after being rescued. Mtoto akiendelea kupatiwa watibabu
 The baby is reportedly in stable condition at the hospital, while local police are investigating the mother, who says she unexpectedly gave birth while sitting on the toilet.
Mtoto aliyeokolewa chooni akiwa anapewa maziwa.

Beijing China
 Wapangaji katika nyumba moja huko Mashariki mwa China walishutuliwa na mlio kama wa sungura au paka na walipoangalia ni nini waliona mguu wa mtoto mchanga ukionekana katika sehemu ya bomba la maji ya chooni. Waokoaji walijaribu kwanza kumvuta mtoto kabla hawajakata kipande cha bomba ili kumwokoa yule mtoto. Baada ya kushindwa kuchomoa kwenye lile bomba hata baada ya kulikata ilibidi wapeleke kipande cha bomba ambamo bado mtoto alikuwa amenasa, katika hospitali ya karibu iitwayo Jinhua. 
Madaktari pamoja na waokoaji walijitahidi kutumia koleo na mikasi hadi kumota kichanga huyo ambaye bado hata kondo lilikuwa bado halijakatwa.
Jana mtoto huyo ambaye anajulikana kama "baby 59" alikuwa anaendelea vizuri na alikuwa akilishwa maziwa.
 

Maajabu ya mama wa mtoto
Mama wa mtoto huyo anatajwa na polisi kuwa na umri wa miaka 22. Polisi wanasema hadi sasa wanaamini maelezo ya huy mama ambaye yeye anadai kuwa alijirikia tumbo kumuuma ghafla na akajisikia kwenda haja kubwa. Hata hivyo siku zake za kujifungua zilishatimia. Mara mtoto akatoka wakati yeye akijisaidia hajakubwa na kutumbukia choooni
Mwanamke huyo aliwaambia maafisa wa polisi kuwa hakukusudia kutupa mtoto huyo chooni ila ilitokea kwa bahati mbaya bila yeye kujua. Hata hivyo mama huyo alijaribu kumvuta mtoto kwa kijiti akashindwa hivyo akaamua kuflash choo ili kuongoa damu lakini mtoto naye akaondoka na maji.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...