Na Ramadhan Libenanga, Morogoro
WAZIRI
Mkuu Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye, amewataka
Watanzania kutambua kwamba hakuna mtu tajiri anayetoa fedha na mali zake
bila masharti; na kuwa iwapo Watanzania watawaweka madarakani viongozi
kwa rushwa, wasitegemee Katiba Mpya itajibu matatizo yao ndani ya jamii.
"Tukumbuke
kuwa anayekuhonga ili umpigie kura akishaingia madarakani mkataba wake
na wewe uliishia pale ulipomuuzia kura yako na yeye kazi atakayofanya
akipata hiyo ofisi au madaraka ni kusaka rushwa na kufisadi mali za umma
ili arudishe fedha zake alizotumia kukununua wewe na wenzako," alisema
Sumaye.