ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI
Showing posts with label ccm. Show all posts
Showing posts with label ccm. Show all posts

Tuesday, March 24, 2015

KINANA AWATAKA VIONGOZI WEZI, MAFISADI KUNG'OKA HARAKA CCM

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na msafara wake ukiwa umezingirwa na wananchi wa jamii ya kimasai ulipokuwa ukiondoka baada ya kuhutubia mkutano katika Kijiji cha Mtakuja, Kata ya Kia, Jimbo la Hai, mkoani Kilimanjaro leo, wakati wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua miradi inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM, pamoja na kusikiliza kero za Wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.

Komredi Kinana ambaye katika ziara yake ameambatana na Katibu wa Itikadiu na Uenezi, Nape Nnauye, ameutaka uongozi wa Kampuni ya Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro kuacha kuwabughudhi wananchi wa kata hiyo, baada ya kutoa mallamiko kuwa unataka kuwapora ardhi iliyo karibu na uwanja huo yenye ukubwa wa zaidi ya hekali 10,000 inayomilikiwa na vijiji 11.

Komredi Kinana amekemea tabia hiyo ya baadhi ya viongozi wanaopora kinguvu ardhi za wananchi. Pia amewahakikishia wananchi hao kuwa atasaidia kurejesha ardhi hiyo kwa kukutana na Rfais Jnakaya Kikwete na kumwambia juu ya dhulma hiyo/

Komredi Kinana , amesema kuwa kiongozi yeyote aliyeingia CCM kwa minajiri ya kutaka kujineneemesha binafsi kimaisha, kwanzia sasa hatakuwa na nafasi na inabidi aondoke katika chama hicho ambacho kazi yake ni kutetea haki za wanyonge.
 Komredi Kinana akishangiliwa na wananchi wa Kijiji hicho cha Mtakuja kinachokaliwa na jamii ya wamasai.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akishangiliwa na wananchi wa Kata ya Kia katika mkutano uliofanyika katika Kijiji cha Mtakuja.

 Wananchi wakishangilia baada ya kufurahishwa na hotuba ya Komredi Kinana.
 Wananchi wa Kata ya Kia, wakimpatia zawadi ya vazi la Kimasai pamoja na fimbo, Komredi Kinana wakati wa mkutano huo.
 Komredi Kinana akihutubia katika mkutao wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Mtakuja, Kata ya Kia, Jimbo la Hai, mkoani Kilimanjaro.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akihutubia mkutano wa hadhara mjini Hai leo. Jimbo hilo linaongozwa na Mbynge, Freeman Mbowe wa Chadema. Amesema mbunge huyo ajiandae kuachia jimbo hilo kwani katika uchaguzi wa mwezi Oktoba CCM mwaka huu itashinda kwa kishindo na kutwaa jimbo hilo
 Wananchi wakisikiliza kwa makini hotuba ya Komredi Kinana mjini Hai wakati wa mkutano wa hadhara.
 Waziri wa Elimu wa zamani, ambaye pia alikuwa waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Israel Nawinga, akimueleza jambo Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alipotembelewa na viongozi wa CCM kumjulia hali nyumbani kwake Losaa, Masama wilayani Hai leo.
 Komredi Kinana akishiriki kuchimba msingi wakati wa ujenzi mpya wa majengo ya Shule ya Msingi Modio iliyopatwa na jangoa la tetemeko na kubomoka eneo la Masama Mashariki, wilayani Hai.
 Watoto wanaosoma Shule ya Awali wakipita bila woga kwenye Daraja la zamani sana la Mnepo liliotengenezwa kwa kamba za waya katika Kijiji cha Kiyungi, wilayani Hai.
 Mmiliki wa Blogu hii, Kamanda Richard Mwaikenda akipita kwa uangalifu kwenye Daraja la zamani la Mnepo, wilayani Hai, Kilimanjaro leo.
 Komredi Kinana akishiriki kupaka rangialiposhiriki ujunzi wa daraja jipya la Mnepo lililojengwa kwa fedha za Serikali takribani sh. bilioni 1 katika Kijiji cha Kiyungi mpakani mwa wilaya za Hai na Moshi Vijijini.
 Komredi Kinana akikagua ujenzi wa Daraja jipya la Mnepo
 Komredi Kinana akipita kwenye daraja la zamani la Mnepo lililojengwa enzi za ukoloni katika Kijiji cha Kiyungi, mpakani mwa Wilaya za Hai na Moshi Vijijini. Daraja hilo limejengwa na kwa waya.
 Komredi Kinana akimkabidhi ng'ombe iliyotolewa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kwa Kijiji cha Kwasadala kilichofanya vizuri katika uchaguzi uliopita hivyo kuipatia CCM ushindi mnono. Pia kijiji hicho kilikabidhiwa gunia moja la mchele.
 Komredi Kinana akihutubia katika mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM Jimbo la Hai.
 Wananchi wakipiga picha za kumbukumbu wakati Komredi Kinana akihutubia katika Kijiji cha Mtakuja, Kata ya Kia, wilayani Hai.
 Komredi Kinana akizungumza na watumishi wa Hospitali ya Wilaya ya Hai, ambapo pia alikagua ujenzi wa chumba kipya cha Xray, katika Mji wa Bomang'ombe, wilayani Hai.
 Komredi Kinana akiijaribu mitambo ya Xray iliyopo katika chumba hicho cha upimaji kwa njia ya mionzi.
 Nape akipigwa mionzi (Xray) ya mkono wake wa kulia
Wauguzi na watumishi wa hospitali ya Wilaya ya Hai, wakiwa katika picha ya pamoja na Komredi

Friday, March 6, 2015

Kufichua mafisadi salama ya CCM- Abdulrahman Kinana

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa Jimbo la Kongwa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Mkoka,wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma ikiwa sehemu ya muendelezo wa ziara zake za kukagua utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya CCM mwaka 2010.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Mkoka wilayani Kongwa na kuwaambia moja ya sifa muhimu na ya kipekee kwa kiongozi anayefaa kuongoza wananchi ni Uadilifu.
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma Mheshimiwa Adam Kimbisa akihutubia wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa hadhara ambao Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alikuwa mgeni wa Heshima, Kimbisa aliwaambia wana CCM kuwa Dodoma itakuwa mfano katika kutenda haki.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Mkoka wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma ambapo aliwaambia wananchi hao CCM ni Chama pekee chenye kujali Watanzania kinachosimamia na kuitunza amani iliyokuwepo
 

Mpwapwa.Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana amesema kitu kitakachokiokoa chama hicho ni wanachama kutowafumbia macho wezi na mafisadi akisisitiza kuwa kulindana na upole kutakiangamiza chama hicho kikongwe.
Kinana amesema hayo wakati CCM ikizidi kuchafuliwa na kashfa za ufisadi ambazo zimekuwa zikiwakabili makada wake ambao mara kadhaa wamelazimika kuachia ngazi baada ya Bunge kukomaa kutaka hatua zichukuliwe.
Tayari makada wa CCM wameshalazimika kuwajibika katika kashfa za uchotwaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow ambako zaidi ya Sh306 bilioni zilichotwa, kashfa ya Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), kashfa iliyoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kashfa ya rada na nyingine kwenye sekta ya utalii.
Tayari makada wa CCM wameshalazimika kuwajibika katika kashfa za uchotwaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow ambako zaidi ya Sh306 bilioni zilichotwa, kashfa ya Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), kashfa iliyoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kashfa ya rada na nyingine kwenye sekta ya utalii.
Kinana, ambaye amekuwa akishambulia viongozi wa Serikali kwenye ziara zake, alitoa agizo hilo juzi wakati alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara kwenye Viwanja vya Kibakwe wilayani Mpwapwa ambako alisema kufanya hivyo ndiyo salama ya CCM.
“Tatizo lenu (wanachama wa CCM) mnakuwa wapole na mnajenga tabia ya kulindana. Kwa njia hiyo hamtaweza kukisaidia chama chenu. Mtu akikosea hakuna bahati mbaya, ondoa huyo na apelekwe jela mara moja ili kazi nyingine zisonge,” alisema Kinana ambaye hata hivyo hujiepusha kuzungumzia kashfa hizo kubwa kwenye mikutano yake.
Kwa upande mwingine alisema kuwa ndani ya CCM kuna baadhi ya wanachama wezi ambao alidai hawajai kiganja kati ya wanaCCM 7 milioni, lakini wamesababisha wanaCCM kudharauliwa na kuwakosesha raha maskini wengi walioko vijijini ambao alisema wanaendelea kutukanwa kuwa ni mafisadi jambo ambalo siyo kweli.
Huku akishangiliwa na umati mkubwa uliohudhuria mkutano huo, alisema dhambi mbaya kwa sasa ni ile ya kufanya kazi kwa mazoea na kulindana kwa kisingizio cha utawala bora wakati wezi wanaiba bila ya kuangalia masuala ya utawala bora.
Kauli ya Kinana huenda ikawapa nguvu baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wakisimama kidete kwa ajili ya kupinga ufisadi, lakini mara kadhaa wakiwa bungeni hushindwa katika mapambano yao kutokana na misimamo ya chama.
Kinana alisema suala la wanachama wa CCM kuimba “iyena iyena” huku wakiwa wapole huu siyo wakati wake badala yake wabadilike na kukemea maovu na mambo yanayokwenda kinyume na chama chao.
 “Nasema kwa wanachama wa CCM nchi nzima, mpango wa kuhamisha mtu kutoka eneo moja na kupelekwa sehemu nyingine huo usiwepo, mtu akituhumiwa lazima aachie ngazi akisubiri uchunguzi,” alisema na kuongeza.
“Wakati wa kuiba wezi hawafuati utawala bora, lakini wanapotakiwa kuondoka ndipo masuala ya utawala bora yanapoanza kusimama, naona suala la utawala bora litazamwe upya maana wengine hawafanyi kama tulivyowatuma.”

Tuesday, January 27, 2015

BREEKING NEWS, MABOMU YATAWALA MBAGALA, PROFESA LIPUMBA AKAMATWA, NI MAANDAMO YA CUF


HABARI zilizotufikia mda huu zinasema Jeshi la Polisi Mkoani Dar es Salaam limetumia nguvu kwa  kurusha mabomu ya machozi ili kuwatawanya wananchama cha Wananchi CUF waliokuwa kwenye maandamo wilaya ya Temeke .
Na kufanikiwa kuwatia nguvuni viongozi waandamizi wa chama cha Wananchi CUF,wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Profesa Ibrahimu Lipumba,huku wananchi wa maeneo hayo wakiishi kwa hofu kubwa sana.
Akithibitisha kukamatwa viongozi hao pamoja na kuvunjwa kwa maandamano .Afisa Habari wa chama cha Cuf ,Bwana Silas  alipoongea na mtandao huu mda huu ambapo amesema waalianza maandamano ya Amani katika Viwanja vya temeke na kwenda mbagala , ambapo maandamano hayo yaliokuwa na lengo la kumbukumbu ya mauaji ya wanachama wao yaliofanyika  TAREHE 26 januari mwaka  2001 huko Zanzibari na Tanzania Bara,
        Bwana Silas alisema wakati wapo kwenye maandamo hayo walipofika maeneo ya Mtongani iliyopo wilaya ya Temeke ndipo Jeshi la polisi likafika na kurusha mabomu na kuwapiga wanachama wa chama hicho na kufanikiwa kuwakamata viongozi wa chama hicho,na kuwapeleke kituo kikuu cha polisi.kwa madai maandamano hayo hayana ruhusa.

Wednesday, July 16, 2014

TAZAMA PICHA 8 ZA WAFUASI WA CHADEMA NA CCM WALIPOCHAPANA MAKONDE JIJINI DAR MBELE YA WAZIRI WA MAJI NA JOHN MNYIKA


 Wafuasi wa CCM na Chadema wakitaka kuzipiga kavu kavu baada ya kutokea mzozo ambapo wanaCCM walikuwa wakimzomea Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika  akihutubia na WanaChadema wakimzomea Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla  akihutubia katika mkutano huo.
 Wafuasi wanawake wa CCM na Chadema wakichimbia mkwara.


 Poilisi wakiwatuliza wafuasi wa Chadema waliokuwa wakipinga Mbunge wao John Mnyika asijibu swali lililoulizwa na Mkazi wa Kibamba, Jordan Balindo aliyemtaka Mnyika aeleze ni jitihada hani amezifanya binafsi kama mbunge kutatua changamoto ya ukosefu wa maji katika jimbo la Ubungo.
 Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azzan wa CCM (KULIA), akiamulia ugomvi wa Diwani wa Kimara, Pascal Manota wa Chadema (kushoto) na Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge waliotaka kuzichapa ulipotokea mzozo katika mkutano wa hadhara wa Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla katika Uwanja wa Shule ya Mavurunza, Kata ya Salanga, Jimbo la Ubungo, Dar es Salaam jana.
 Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla (kushoto) na Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika (Chadema), wakitofautiana jukwaani wakati Makalla akiamuru polisi kuwatoa wafuasi wa Chadema waliokuwa wakimzomea wakati akileleza Utakelezaji wa Ilani ya CCM JUU YA MAJI, HUKU mNYIKA AKITAKA WAENDEE KUZOMEA AKIDAI KWAMBA WAZIRI HAKUFANYA HAKI KWANI YEYE ALIPOKUWA AKIZOMEWA NA WANA CCM HAKUWACHUKULIA HATUA KAMA HIYO KATIKA MKUTANO WA HADHARA ULIOFANYIKA KATIKA UWANJA WA SHULE YA MAVURUNZA, KATA YA SALANGA

 Mfuasi wa CCM  akiwa na bango la kumshutumu Mbunge wa Jimbo hilo, John Mnyika.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Taka, Dar es Salaam, EvaSinare (katikati) akijaribu kuunusuru mzozo huo kwa kuzungumza na Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla 9kushoto) na Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika.
Mfuasi wa Chadema akiwa na bango la kuishutumu Serikali
 Polisi akilinda usalama mbele ya mashabiki wa CCM na Chadema

 Mbunge wa Jimbola Kinondoni, Idd Azzan akihutubia katika mkutano huo

 Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akihutubia kwakueleza utekelezaji wa Ilani ya CCM, ambapo aliwahakikishia wananchi wa  jiji la Dares Salaam kwamba ifikapo mwishoni mwa mwaka ujao tatizo la maji litakuwa historia hasa baada ya kukamilika upanuzi wa Mtambo wa Maji wa Ruvu Juu ambao ujenzi wake umeanza sasa.
 Makalla akipata maelezo kutoka kwa mkandarasi kuhusu ujenzi wa Tanki jipya la maji eneo la Kibamba, Dares Salaam,wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maji Dares Salaam na Pwani.
 Mkazi wa Kibamba, Chrisant Kibogoyo akiuliza swalikatika mkutanouliofanyika Kata ya Kibamba.
 Mwalimu wa Shule ya Msingi ya Kibwegere, Hellen Mshana akiuliza swali kwa waziri kwambanilini maji yatasambazwa katika shule hiyo na zinginezo
 Askari akimuondoa mfuasi wa Chadema aliyekuwa akilazimisha kumuuliza swali Waziri Makalla katika mkutano huo.
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Maji Safi na Taka Dares Salaam, (Dawasco), Jackson Midalla akijibu moja ya maswali yaliyoulizwa na Diwani wa Kata ya Kibamba, Issa Mtemvu wakati Waziri Makalla, alipotembelea mradi wa maji katika kata hiyo.
Wafuasi wa CCM  na Chadema wakishindana kupeperusha bendera za vyama vyao wakiwakwenye magari eneo la Kibamba. PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG

Monday, May 5, 2014

Kinana aunguruma Pemba


 
Katibu Mkuu wa CCM,Ndg. Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa Mikoa miwili ya Kisiwani Pemba waliofurika kwa wingi kwenye Mkutano wa Hadhara wa Chama cha Mapinduzi uliofanyika jioni ya leo kwenye Viwanja vya Gombani ya Kale,Kisiwani Pemba.Katika hobuba yake,Ndg. Kinana amewataka Wananchi wa Kisiwani humo,kutohadaika na Wanasiasa wanapita kila mahali kwa lengo la kulipotosha Taifa,hasa juu ya swala la Muundo wa Serikali katika Mchakato wa Katiba Mpya.
35
Katibu Mkuu wa CCM,Ndg. Abdulrahman Kinana akiendelea kuwahutubia wananchi wa Mikoa miwili ya Kisiwani Pemba waliofurika kwa wingi kwenye Mkutano wa Hadhara wa Chama cha Mapinduzi uliofanyika jioni ya leo kwenye Viwanja vya Gombani ya Kale,Kisiwani Pemba.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar,Ndg. Vuai Ali Vuai akizungumza na wananchi wa Mikoa miwili ya Kisiwani Pemba waliofurika kwa wingi kwenye Mkutano wa Hadhara wa Chama cha Mapinduzi uliofanyika jana kwenye Viwanja vya Gombani ya Kale,Kisiwani Pemba.
Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye akiwapa somo wananchi wa Mikoa miwili ya Kisiwani Pemba waliofurika kwa wingi kwenye Mkutano wa Hadhara wa Chama cha Mapinduzi,uliofanyika kwenye Viwanja vya Gombani ya Kale, Kisiwani Pemba.
Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye akiendelea kuzungumza.
Makamu Mwenyekiti UWT,Bi. Asha Bakari Makame akizungumza kwa msisitizo mkubwa na wananchi wa Mikoa miwili ya Kisiwani Pemba waliofurika kwa wingi kwenye Mkutano wa Hadhara wa Chama cha Mapinduzi,uliofanyika kwenye Viwanja vya Gombani ya Kale, Kisiwani Pemba.

Naibu Katibu Mkuu UVCCM Zanzibar,Ndg. Shaka Hamdu Shaka akizungumza machache na wananchi wa Mikoa miwili ya Kisiwani Pemba waliofurika kwa wingi kwenye Mkutano wa Hadhara wa Chama cha Mapinduzi,uliofanyika jioni ya leo kwenye Viwanja vya Gombani ya Kale,Kisiwani Pemba.

Vijana wa CCM, Fatma Juma Ramadhan (kushoto) na Halima Juma Hajj wakighani mashairi mazuri ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM,Ndg. Abdulrahman Kinana (hayupo pichani).
Sehemu ya picha mbali mbali za wananchi wa Mikoa miwili ya Kisiwani Pemba wakifuatilia Mkutano wa Hadhara wa Chama cha Mapinduzi,uliofanyika jioni ya jana kwenye Viwanja vya Gombani ya Kale,Kisiwani Pemba.(Picha zote na Othman Michuzi).
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...