ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Wednesday, October 31, 2012

Kimbunga Sandy Kinavyoendelea kuitesa Marekani

 
Uharibifu uliofanwa na kimbunga Sandy  New York City

  
Kazi ya usafi sambamba na uokozi inaendelea katika majiji mbalimbali Marekani

 
Jiji la New jersey lilivyoharibiwa
 
Nyumba zaidi ya mia moja zimewaka moto ukiachilia mbali magari na mali nyingine

  
Wananchi wakiangalia mabaki ya nyumba zao
 
Barabara zote za chini zimejaa maji

  
Mtoto akiokolewa maeneo ya Manhattan, New York
  
Njia za reli na barabara sikiwa zimeharibiwa vibaya
 
Watu wakiendelea kuokolewa New York

 
Jiji la Toronto linavyoonekana leo

 
Nyumba bado zimezungukwa na maji Grassy Sound kaskazini mwa Wildwood, New York 
 
  
Boti iliyojikuta katikati ya njia za reli baada ya kimbunga Sandy

 Gallery Photo

 
New York Financial District

 
 usatoday 
Yadi ya magari ikiwa imefunikw ana maji


mikeyzimzimmer 
Kazi  ya usafi imeanza.

Vifo vinavyoendelea kuripotiwa kufuatia kimbunga Sandy kilichoikumba miji ya Pwani ya MAshariki ya Marekani vinaendelea kuripotiwa. Moto uliozuka baada ya kimbunga hicho umeunguza nyumba takribani 100 katika eneo la Breezy Point Queens. Milipuko na kukatika kwa nyaya za umeme zimeacha eneo ya Manhattan (eneo ambapo Al Queda walilipua majengo pacha) lilikuwa bila umeme kwa asilimia 90. Barabara za chini ya ardhi za New York ambazo husafirisha mamilioni ya watu zimejaa maji na haijulikani ni lini zitafunguliwa.
Ajali katika maeneo mbalimbali zime sababisha vifo vya watu 40 hadi sasa kuanzia Marekani hadi Canada. Watoto wawili wa kiume Little wa kati ya miaka 11 na 13 walikufa baada ya nyumba yao kuangukiwa na mti mkubwa Salem New York. Askari mmoja aliyekuwa likizo lakini akajitosa kuwaokoa watoto hao naye alikufa ndani ya nyumba hiyo baada ya kuwaokoa watu wengine pamoja na mtoto wa miezi 15.

 

Rais Obama ameidhinisha mfuko wa maafa wa kitaifa kusaidia katika kujenga upya miundombinu ya miji ya New York na New Jersey Obama alisema “All of us have been shocked by the force of mother nature,” said the president, who plans to visit New Jersey on Wednesday. He promised “all available resources” for recovery efforts.
Waokoaji wameendelea kutafuta watu walionusurika katika mkasa huo katika miji ya Atantic na kwingineko. RAis Obama aliongena na Magavana 20 na Mameya wa miji iliyoathirika kwa simu na Ikulu ya White House imesema itafanya tathmini ya uharibifu uliotokea pamoja na Mr. Christie wa Republican ambaye amekuwa akimtuhumu Rais Obama kwa kutofanya vizuri katika kukabiliana na janga la kimbunga hicho.

TAfsiri na: Richard Bahati


No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...