ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Sunday, October 14, 2012

Syria sasa inatumia mabomu ya CLUSTER

Shirika la kimataifa la kutetea haki za kibinaadamu, Human Rights Watch, limeishutumu Syria kuwa inazidi kutumia mabomu chane, yaani cluster bombs, dhidi ya raia.

 
Vibomu vidogo vidogo vinakuwa kwenye bomu kubwa
 Bomu na vibomu vyake ambavyo havijalipuka
 
Bomu likeshaachiliwa hulipua vile vibomu vidodo vidogo na husambaa eneo kubwa sana
Vita vya Syria 
Syria inavyoonekana leo baada ya mabomu ya Cluster kuanza kutumiwa na Serikali dhidi ya raiya
 
Mlipuko wa Cluster Bomb
 
Majeruhi wa Cluster bomb: Momu hili lina uwezo wa kumchana chana mtu vipande vipande
Shirika hilo linasema limeangalia video kwenye mtandao zinazodai kuonesha mabomu kama hayo 20 yakitumiwa sehemu mbali-mbali za Syria katika juma lilopita, ikilinganishwa na mwaka mmoja na nusu uliotangulia.
Akizungumza jana, mkurugenzi wa Umoja wa Mataifa wa Human Rights Watch, Philippe Bolopion, alisema inaonesha kuwa serikali haiwatii maanani kabisa wananchi wa Syria.
"Kwa muda tumekuwa tukishuku kuwa serikali ya Syria inatumia mabomu ya chane (yaani cluster bomb) lakini sasa tuna video na mashahidi kwamba serikali imetupa mabomu kama hayo kwenye maeneo ya makaazi kwa kutumia helikopta.
Kwa mfano imerusha mabomu hayo baina ya shule mbili.
Kwa hivo tunaamini kuwa serikali ya Syria inafaa kuacha haraka kutumia silaha za hatari zisokubalika kama hizi na isafishe maeneo yote ambako mabomu hayo yamemwagwa, na piya iwaarifu wakaazi wahusika juu ya hatari ya vibomu vidogo vilivotawanyika".

Source:  http://www.bbc.co.uk/swahili

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...