ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Friday, October 12, 2012

VURUGU ZENYE MWELEKEO WA KIDINI - MBAGALA


Taarifa zilizotufikia hivi punde zinaeleza kwamba kuna vurugu kubwa Mbagala, jijini Dar es Salaam zenye mtazamo wa kidini, ambapo makanisa matatu yanadaiwa kuchomwa moto
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
  Baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu wakikizingira Kituo cha Polisi cha Maturubai kilichopo Mbagala jijini Dar leo.
    Baadhi ya maafisa wa polisi wakinawa maji baada ya mabomu ya machozi kupigwa.
   Gari la  Kampuni ya Clouds Media Group likiwa limepasuliwa kioo cha nyuma.
  Jamaa aliyejitambulisha kwa jina la Ally Ramadhani ambaye ni dereva wa daladala naye akiwa ameambulia kipigo baada ya kujichanganya na waandamanaji.
    …Dereva Ally Ramadhani akisikilizia maumivu.
     Mmoja wa waandamanaji.
     Baadhi ya waandamanaji wakiwa wamewekwa chini ya ulinzi.
Kanisa la Sabato Mbagala Kizuiani likiwa limevunjwa vioo.
…Vioo vilivyovunjwa kanisani hapo.
…kanisa hilo la Sabato.
  ...Muonekano wa kanisa hilo la Sabato.
    Jamaa aliyejitambulisha kwa jina la Paul Martin ambaye alidai alikuwa akienda sokoni ndipo akaambulia kipigo.
Kanisa la Aglikana ambalo pia lilishambuliwa na waandamanaji.
…Anglikana.
   Mabenchi ya kanisa la Anglikana yakiwa yametupwa nje.
Kibao cha kanisa kikiwa kimevunjwa.
  Muonekano wa kanisa hilo la Anglikana.
Gari lililokuwa ndani ya Kanisa la T.AG Mbagala Kizuiani likiwa limevunjwa vioo.
…Hili lilichomwa moto.
Baadhi wa waumini wa kanisa la T.A.G wakililinda kanisa lao.
---
WATU wanaodaiwa kuwa ni Waislamu wamevamia makanisa mbalimbali yaliyopo Mbagala Kizuiani jijini, Dar wakihamasisha vurugu wakimtuhumu mtoto Emmanuel Josephat kuwa amekojolea kitabu cha dini hiyo (Msaafu) Oktoba 10, mwaka huu.
Baadhi ya makanisa yaliyoshambuliwa ikiwa ni pamoja na kuchomwa moto magari yao ni  Kanisa la Sabato, Aglikana na T.AG .
(PICHA/HABARI: ERICK EVARIST/GPL)


Wacha waue watu wote tuone wao watabaki na nani... Huwezi kumpenda Mungu usiyemuona ukamuua na kumchukia binadamu unayeishi naye huo ni unafiki, chuki na ubinafsi. Dunia inashuhudia mataifa yanayojiita ya kidini yakiwa yanapigana na tena vita ya wenyewe kwa wenyewe pamoja na kuwa ni dini moja. Upo wapi upendo Mungu yupi tunamwamini?? Unachoma makanisa na kuua watu kwasababu ya udini, chuki na ubinafsi. Inasikitisha sana Tanzania ya leo badala ya kukabili umaskini, maradhi na ujinga, tunakabili DINI tena tuliyoletewa na wazungu na waarabu?
Leo utaua mkristo, kesho utaua mpagani na kwakuwa umezoea kuua keshokutwa utamuua mwislam mwenzio kwakuwa umezoea kuua na wakristo vivyohivyo. Tunashuhudia hayo somalia, afghanistan, tunisia, mali, libya, iraq na nyinginezo.
Tujaribu kubadilika, tutumie dini kuweka mahusiano yetu na mwenyezi Mungu maana hakuna liyewahi kupata manufaa kwa kumchukia mtu, wanaoeneza chuki za dini kwa kigezo cha wao na sisi eti au elimu na kuzidiana hakujengi taifa. Tafakari maisha ya vizazi vyetu vijavyo wataishi taifa lipi la watu wasioelewana??
Nawasilisha,
mzalendo.
cosmasalex@yahoo.com

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...