ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Sunday, December 30, 2012

Msichana aliyebakwa na wanaume sita India Afariki dunia


 
Mwili wa msichana aliyebakwa hadi kufa ukiingizwa kwenye gari 

Maandamano India
Raia wa India wakiandamana 
 
 
 Mishumaa imewashwa nchinii nyesha mshikamano wa kukataa Ubakaji
  

  
  
Bango linalotaka wabakaji wapewe adhabu ya kukatwa nyeti zao
 
Wanaume nao waandamana nakusema "Mwanaume wa Kweli habaki"
  
Mwandamanaji akilia kwa uchungu  baada ya kupata taarifa za kifo cha msichana aliyebakwa na wanaume 6
 
Watoto nao hawako nyuma kwenye kulilia haki za wasichana wanaobakwa mara kwa mara India

Tunalaani
 
 
Waombolezaji wakilia na kusali
 

 Askari wa kutuliza ghasia wakijaribu kutawanya waandamanaji
  
 

 
Wanaume wakilala chini kama wamekufa wakionyesha mshikamano kupinga ubakaji
 

  
  
Watoto wa shule nao washiriki maandamano
 
 
 
Ghasia zaendelea kuzagaa katika majiji ya Dheli, Calcuta, Mumbai na Bangalore
 
Mali zaharibiwa na waandamanaji
  

 
Jeneza lenye mwili wa Msichana (jina limehifadhiwa) hadi kufa likiwa tayari kurudishwa India kutoka Singapore alikopelekwa kufanyiwa matibabu maalum (hata hivyo alifariki dunia)
 
 
Habari kamili 
Maelfu ya watu wamejiunga katika maandamano ya amani katika mji mkuu wa India, Delhi, kupinga kitendo kilichosababisha kifo cha mwanamke mmoja ambaye alibakwa na kundi la wanaume mjini humo.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 23, ambaye bado hajatambuliwa, amekufa kutokana na na majeraha Jumamosi huko Singapore alikopelekwa kupata matibabu maalum.
Wanaume sita wanaoshikiliwa kuhusiana na tukio la kumbaka mwanamke huyo, sasa wamefunguliwa mashitaka ya mauaji.
Shambulio hilo la aibu lilifanyika tarehe 16 Desemba 2012 na kusababisha maandamano kupinga unyanyasaji wanaofanyiwa wanawake nchini India.
Maafisa wawili wa polisi tayari wamesimamishwa kazi.
Mwili wa mwanamke huyo unarejeshwa India katika mazishi yatakayofanyika kwa siri kuepusha ghasia zaidi za waandamanaji.
"Kwa kweli wanawake wengi nchini India wanakabiliwa na kitisho katika maisha yao katika mambo mbalimbali kama vile kunapozuka ghasia, ukosefu wa huduma za afya, kukosekana kwa usawa, kupuuzwa, lishe duni, kutojaliwa kwa afya ya mtu na utu wake"
Polisi wa kuzuia ghasia wamefunga eneo la katikati ya Delhi ili kuzuia maandamano zaidi.
Waziri mkuu wa India Manmohan Singh amesema anaelewa hasira ya wananchi, ametaka hatua zaidi zichukuliwe ili kufanya India kuwa mahali salama kwa wanawake kuishi.
Maandamano pia yamefanyika katika miji mingine ya India ikiwemo Calcutta, Bangalore na Mumbai.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...