ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Thursday, December 6, 2012

Rais wa Misri Mohammed Morsi aikimbia Ikulu yake kwa muda



Waandamanaji wakipambana na polisi

 
Waandamanaji wakirusha mabomu ya petroli

 

waandamanaji wakizunguka viunga vya Ikulu Jiji ni Cairo

 

 

Waandamanaji wakipambana na polisi

 

Polisi wakiwa tayari kukabiliana na waandamanaji

 

Mwandamanaji akijiandaa kurusha bomu la machozi

 

Ukuta uliokuwa ukizuia waandamanaji kuingia ikulu ambapo hata hivyo ulivunjwa na waandamanaji

 

Makabiliano ya uso kwa uso na polisi

 

Wafuasi na wapinzani wa Rais Morsi wakitwangana

  

Waandamanaji wakichoma moto magari na malinyingine



Makabiliano yamezuka kati ya wafuasi wa Rais wa Misri Mohammed Morsi na wapinzani wake nje ya ikulu ya rais mjini Cairo.
Wafuasi wa rais huyo wameharibu mahema yaliyowekwa nje ya ikulu hiyo na wapinzani wa Morsi walioanza kukesha nje ya ikulu hiyo Jumanne kupinga mamlaka aliyojilimbikizia.
Pia wanapinga rasimu ya katiba mpya ambayo itapigiwa kura ya maoni tarehe 15 mwezi Disemba
Makamu wa rais Mahmoud Mekky,amesema kuwa mabadiliko yaliyofanyiwa katiba hiyo yanaweza kukubalika na upinzani.
Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani,Hillary Clinton amesema mazungumzo yanahitajika haraka kuhusu katiba hiyo.
Maelfu ya wapinzani wa rais wameapa kuendelea na maandamano yao nje ya ikulu ya rais mjini Cairo.
Baadhi wameweka mahema nje ya ikulu na sasa wanuzunguka ukuta wa ikulu hiyo.
Maelfu wameizingira ikulu wakimpinga rais kwa kujilimbikizia mamlaka
Siku ya Jumanne , maelfu ya waandamanaji walivamia ikulu wakipinga rasimu ya katiba iliyozua utata mkubwa pamoja na kupinga sheria inayomlimbikizia mamlaka makuu Rais Morsi.
Wakati mmoja polisi walifyatua gesi ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji hao ambao walikuwa wamevuka ukuta wa seng'enge.
Vikosi vya usalama vilitoa taarifa vikisema kuwa rais Morsi ameondoka katika ikulu hiyo na ameomba utulivu.
Waandamanaji hao wanapinga hatua ya rais kujilimbikizia madaraka mapya na kusababisha kuundwa kwa rasimu ya Katiba.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...