ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Monday, April 8, 2013

Chadema kuwasha moto bungeni, ni kuhusu wanachodai 'utendaji usiofaa' wa Bunge


 


   Dar es Salaam. Wakati Bunge la 11 la Bajeti kwa mwaka huu likianza kesho, Kamati Kuu ya Chadema imesema itatumia Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kulibana Bunge kuhusu utendaji usiofuata Kanuni za Bunge unaofanywa na Spika na wasaidizi wake.
Pia wabunge hao wameitaka Serikali kuweka wazi mikataba iliyoingia hivi karibuni na Serikali ya China ili wananchi waweze kufahamu kilichomo vinginevyo watatumia kambi hiyo kuwabana wahusika.
Katika kikao cha 10 kilichomalizika Februari 8, mwaka huu mjini Dodoma, Mnadhimu wa kambi hiyo, Tundu Lissu alisema kuwa wanaandaa hoja za kumng’oa Spika na Naibu wake, Job Ndugai kwa kile walichodai kukiuka kanuni mbalimbali za Bunge.
Kambi ya upinzani ilikuwa ikilalamika kuondolewa kwa hoja binafsi za baadhi ya wabunge wao ikiwemo ya Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (Maji), James Mbatia (Mitalaa ya Elimu) na Joshua Nassari, ambaye hoja yake ilihusu utendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA).
Hata hivyo, Spika wa Bunge, Anne Makinda wakati akiahirisha kikao cha 10, alisema kuwa hoja binafsi zitakuja tena katika kikao cha 11 na wenye hoja watazifufua.
Jana, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika alisema Kamati Kuu ilibaini kwamba matukio yaliyotokea katika kikao 10 yalitokana na meza ya spika kutofuata kanuni.
“Tumeamua kwamba Kambi ya Upinzani Bungeni itashughulikia tatizo hili la upindishwaji wa kanuni za Bunge ili wahusika wabanwe kwa vitendo wanavyovifanya,” alisema.
Alisema kambi hiyo itafanya hivyo kwa kufuata sheria na miongozo ambayo inawabana watendaji hao wa Bunge ili waweze kuwajibishwa kwa vitendo vyao.
Akizungumzia mikataba, Mnyika alisema kamati hiyo ina wasiwasi kuhusu mikataba 17 iliyoingiwa na Serikali za Tanzania na China na kutaka iwekwe hadharani.
Baadhi ya mikataba iliyotiwa saini ni katika kilimo, sekta ya afya, miundombinu ikiwamo mkataba wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo mkoani Pwani, ujenzi wa Reli ya Kati na ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara), kwenda maeneo mbalimbali nchini hali itakayorahisisha usafirishaji wa mizigo.
Mikataba mingine ni uboreshaji wa sekta ya viwanda, kilimo hasa cha tumbaku na kulipatia Shirika la Utangazaji Tanzania zana za kufanyia kazi.
“Kamati Kuu inaitaka Serikali kuweka wazi mikataba hiyo vinginevyo watataka ufafanuzi katika kikao cha Bunge la Bajeti kinachotarajia kuanza rasmi kesho.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...