ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Thursday, May 9, 2013

SHEKHE ISSA PONDA AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MWAKA MMOJA NJE HUKU WENZAKE WOTE 49 WAKIACHIWA HURU NA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU JIJINI DAR ES SALAAM LEO


 katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiisilamu Tanzania Sheikh Ponda Issa Ponda akisindikizwa na askari muda mfupi baada ya kuachiwa
katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiisilamu Tanzania Sheikh Ponda Issa Ponda Akihojiwa na mmoja wa waandishi wa habari!
Mhadhiri Maarufu wa Kiisilamu Sheikh Habibu Mazinge (suti nyeusi) akimlaki Sheikh Ponda mara baada ya kuachiliwa huru.
Ponda akizungumza na waandishi wa habari.
 katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiisilamu Tanzania Sheikh Ponda Issa Ponda akitoka nje ya jengo la mahakam ya hakimu mkazi kisutu
Mmoja wa ndugu wa mtuhumiwa akilia baada ya kumkumbatia nduguyake kutokana na kushinda kesi hiyo.
Waumini wa Kiislamu wakiwa Wammbeba Juu mmoja wa aliyekuwa mshtakiwa mwenza na Shekhe Ponda Mara baada ya Kuachiwa Huru leo Katika Mahakama Ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Waandishi nao walifanya mahojiano na baadhi ya washtakiwa na ndugu wa washtakiwa hao.
Akaingia kwenye gari!
Polisi wakiwa wamejipanga kwa tahadhari yoyote ambayo ingeweza kujitokeza
Ulinzi wa Ponda wakati wa kuondoka mahakamani hapo baada ya kuachiliwa.
Msafara ukavamiwa na wafuasi baada ya dereva wa gari lake kusimamisha awasalimie wafuasi hao jambo ambalo polisi walikuwa hawalitaki na kuzua mabishano mazito kwenye mataa ya Maktaba Square.
 Wafuasi wakivamia gari kumsalimia baada ya dereva wa gari hilo kulisimamisha huku polisi wakimvamia aliondoe gari hilo haraka.
Wafuasi wakajimwaga barabarani.Picha na Habari na Mdau Audifance Jackson
--
HATIMAYE katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiisilamu Tanzania Sheikh Ponda Issa Ponda na wafuasi wake 49 leo wameachiliwa huru na mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kufuatia kushinda mashtaka yote yaliyokuwa yakiwakibili na kuonekana hawana kesi ya kujibu. Hata hivyo Sheikh Ponda amehukumiwa kifungo cha Mwaka Mmoja nje kutokana na utetezi wake kuonyesha kulikuwa na nia yakutenda kosa hilo.

Mara baada ya kutolewa hukumu hiyo mahakamani hapo paliibuka shangwe za furaha kutoka kwa mamia ya wafuasi wake waliokuwa wamejazana karibu na eneo la Mahakama hiyo.
 
Pamoja na maelezo yote aliyoeleza Jaji aliyesoma hukumu hiyo alifafanua mambo mbalimbali kuhusu kiwanja kinachodaiwa na waisilamu hao.
 
1.Mahakama hiyo haina uwezo wakuzungumzia mmiliki halali wa kiwanja kutokana na masuala ya migogoro ya aridhi kuwa na mahakama yake ingawa imegundua kuna tatizo la umiliki.
 
2.Upande wa Serikali hakuwa na hoja ya kisheria wala ushahidi wa kutosha wakuwatia hatiani watuhumiwa.
 
3. Hati ya Mashataka ilikuwa na mapungufu mengi ya kisheria.
 
4.Hakimu awaonyesha njia yakudai mali hiyo waislamu kutokana na kile alichodai mali ya wakfu huwa haiuzwi wala haibadilishwi matumizi yaliyokusudiwa.

5.Upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha kwamba watuhumiwa waliopo mbele ya mahakama ni wafuasi wa sheikh Ponda. Awasihi Waislamu kufuata taratibu za kisheria ili kuipata mali hiyo halali itumike kwa madhumuni yaliyokusudiwa.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...