Morogoro.
Maaskofu wa Kanisa Katoliki nchini wameitaka Serikali kutumia njia ya mazungumzo kumaliza migogoro, badala ya kutumia jazba na nguvu.
Maaskofu wa Kanisa Katoliki nchini wameitaka Serikali kutumia njia ya mazungumzo kumaliza migogoro, badala ya kutumia jazba na nguvu.
Vilevile, wamesema kuwa hawako tayari kukaa kimya
huku wakiona amani na utulivu nchini ikivurugika, badala yake
wataendelea kusema ili amani na utulivu viweze kurejea.
Kauli hiyo imekuja baada ya Rais Jakaya Kikwete,
kuwataka maaskofu hao na viongozi wengine wa dini nchini kuendelea
kuisaidia Serikali katika kuimarisha amani na upendo miongoni mwa
wananchi.
Akizungumza wakati wa kuadhimisha Jubilee ya miaka
25 ya uaskofu wake kwenye sherehe zilizofanyika jana katika Seminari ya
Mt Peter mjini Morogoro, Askofu wa Jimbo la Morogoro, Telesphor Mkude,
alisema meza ya mazungumzo ni lazima itumike katika kuimalisha amani na
upendo wa Watanzania badala ya kutumia jazba na nguvu.
Mkude alisema kwa hivi sasa kumeibuka mivutano ya
kidini na kisiasa na kutoa mfano wa vurugu zilizoibuka wilayani
Sengerema mkoani Mwanza juu ya nani ana haki ya kuchinja au kutokuchinja
kati ya waumini wa madhehebu ya Kikristo na Waislamu.
Pia vurugu za mikutano ya kisiasa, makanisa
kuchomwa, mapadri na watumishi wengine kuuawa na kuteswa, kutupwa kwa
mabomu katika mikusanyiko ya watu ikiwamo makanisa na kwamba yote hayo
yangeweza kumalizwa katika meza ya mazungumzo.
Vurugu kubwa zilitokea Jumamosi iliyopita mjini
Arusha baada ya mtu ambaye bado hajajulikana, kutupa bomu katika mkutano
wa Chadema wa kampeni ya uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika katika
viwanja vya Soweto na kuua watu wawili na wengine zaidi ya 60
kujeruhiwa.
Mei 2, mwaka jana, Mwandishi wa Kituo cha
Televisheni cha Channel Ten, Daud Mwangosi aliuawa kwa kulipuliwa na
bomu na askari polisi katika vurugu zilizotokea katika eneo la Nyololo
mkoani Iringa.
Februaria 18, mwaka huu, Padri wa Kanisa Katoliki
Parokia ya Minara Miwili, Mji Mkongwe, Zanzibar aliuawa kwa kupigwa
risasi asubuhi wakati akienda kuendesha misa katika Kanisa la Mtakatifu
Theresia eneo la Mtoni. Mtuhumiwa wa tukio hilo, Omar Musa Makame,
anaendelea na kesi mahakamani kujibu tuhuma za mauaji.
Tukio lingine ni lile la watu wawili kuuawa na
polisi mjini Songea, Februari 22, mwaka jana, wakati wakizuia maandamano
ya wananchi wenye hasira kali waliokuwa wakipinga mauaji yanayohusishwa
na imani za kishirikiana.
Hivi karibuni maaskofu hao walitoa tamko la kuitahadharisha Serikali, kudhibiti vurugu za kidini na kisiasa nchini.
Walionya kuwa iwapo vurugu hizo hazitadhibitiwa huenda nchi ikaingia katika machafuko
No comments:
Post a Comment