Sakata
la kufukuzwa kwa madiwani nane wa chama cha mapinduzi(CCM) Mkoani
Kagera limechukua sura mpya baada ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM
Taifa anayeshughulikia itikadi na uenezi Nape Nnauye kusema madiwani
hao waliosimamishwa wanapaswa kuendelea na kazi zao kama kawaida na ni
madiwani kisheria kutokana na kikao cha Halmashauri kuu ya Mkoa wa
Kagera kutokuwa na mamlaka ya moja kwa moja kuwafukuzisha uwanachama
madiwani hao
Bwana
Nape amefafanua kuwa kwa mujibu wa utaratibu wa kutoa adhabu kwa
viongozi wa CCM walio kwenye vyombo vya dola hasa wabunge na madiwani
kuwa uamuzi wa Halmashauri kuu ya Mkoa siyo wa mwisho na uamuzi huo
unapaswa kupata baraka za Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ndipo
utekelezwe,hivyo madiwani hao ni halali mpaka kikao cha kamati kuu ya
halmashauri kuu ya taifa kitakachoketi tarehe 23 Agosti ambacho kitatoa
maamuzi kuhusu suala hilo.
No comments:
Post a Comment