ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Monday, September 9, 2013

Rais Kikwete azindua mradi wa kufua umeme na ahutubia maelfu ya wananchi jijini Mwanza


 Maelfu ya wakazi wa Mwanza na miji ya jirani wakimsikiliza Rais Kikwete katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza leo jioni.
 Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia maelfu ya wakazi wa Mwanza na miji ya jirani katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza leo jioni.Rais Kikwete yupo Mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa na kubonyeza kitufe kuashiria kuzindua mradi wa kufua umeme wa megawati 60 huko Nyakato,Mwanza leo asubuhi.Kushoto ni Waziri wa Nishati na madini Profesa Sospeter Muhongo.Uzinduzi wa mitambo hiyo ni sehemu ya ufumbuzi wa tatizo la umeme uliokuwa unaikabili kanda ya ziwa.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua mitambo ya kufua umeme wa megawati 60 muda mfupi baada ya kuzindua mitambo hiyo huko Nyakato Mwanza leo. 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete (kulia akiwa na mavazi maalumu) akikagua jengo la upasuaji katika hospitali ya wilaya ya Nyamagana,Mkoani mwanza leo mchana.Picha na Freddy Maro


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumapili, Septemba 8, 2013, amezindua mtambo wa kufua umeme kiasi cha megawati 60 katika eneo la Nyakato mjini Mwanza, umeme ambao utachangia kwa kiwango kikubwa kupunguza shida ya umeme katika Mkoa wa Mwanza na mikoa ya jirani.
 
 
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifungua rasmi jengo la zahanati ya Kata ya Lugeye huko wilayani Magu terehe 7.9.2013.
 Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Kanali Mstaafu wa Jeshi, Shadrack Faustino Mbilizi aliyehudhuria sherehe za ufunguzi wa jengo la zahanati ya Lugeye huko Magu na pia alipokea kupokea kadi yake ya kitambulisho cha matibabu kwa wazee.
Rais Jakaya Kikwete akipokea kitambulisho cha matibabu kwa wazee kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Magu Mheshimiwa Jaqueline Liana kwa ajili ya kupewa Kanali Mstaafu Shadrack Mbilizi na mkewe Mariam Said wakati wa sherehe za ufunguzi wa jengo la zahanati ya Lugeye tarehe 7.9.2013.Picha zote na John Lukuwi

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...