ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Wednesday, October 9, 2013

Mgomo wa wenye mabasi wasababisha usumbufu kwa abiria.


 
 
Mgomo wa wenye mabasi wasababisha usumbufu kwa abiria.
 Mgomo wa kusafirisha abiria katika kituo cha mabasi ya mikoani na nchi jirani cha Ubungo jijini Dar-es-Salaam,umezua usumbufu kwa abiria ambao wamecheleweshwa kwa saa kadhaa kufuatia mgogoro kati ya wamiliki wa mabasi kupinga utekelezaji wa sheria ya viwango vya uzito unaoruhusiwa kwenye barabara za hapa nchini .

ITV ilifika kituoni hapo majira ya alfajiri ili kushuhudia mgomo uliokuwa umeitishwa na chama cha wamiliki wa mabasi ya kusafirishia abiria Tanzania Taboa, kufuatia serikali kupunguza uzito wa asilimia tano kwa  mabasi na malori kwa asilimia tano yatakayokuwa yakitumia barabara za hapa nchini, wakiongea na ITV baadhi ya abiria walikuwa wasafiri na mabasi hayo,wamehoji uhalali wa wao kukatiwa tiketi za safari na mawakala wa mabasi hayo,ili hali wakijua kuwa,matajiri wao wamepanga kuendesha mgomo huo hivyo kuwasababishia usumbufu usio wa lazima.

Naibu katibu mkuu wa TABOA bwana Severine Ngalo amesema kuwa watasitisha ukatishaji tiketi kwa abiria kama serikli itashikilia msimamo huo,na kudai kuwa katika nchi za afrika mashariki hakuna utaratibu wa mabasa ya abiri kupimwa katika mizani barabarani huku wakisema kuwa uataratibu huo unakwamisha ushindani wa soko katika nchi za Africa mashariki.

Afisa katika chama cha kutetea abiria Tanzania bwana Gervas Lutaguzinda amesema kuwa,wamiliki hao wasitumie abiria kama ngazi ya kufikishia matatizo yao kwa serikali,huku mkurugenzi wa barabara toka mamlaka ya udhibiti wa uasfiri wa majini na nchi kavu Sumatra wakidai kuwa watawafutia leseni wamiliki watakao kiuka mkataba wao na mamlaka hiyo.

amesema hatabadilika kwani anasimamia sheria na anayetaka kugoma aendelee kugoma lakini asipeleke gari lake barabarani,hadi ITV inaondoka katika eneo la tukio katika kituo cha mabasi Ubungo mabasi ya abiria yalikuwa yameanza kuondoka kituoni hapo majira ya saa tatu asubuhi,kukiwa na makubaliano ya kutokupitia sehemu za mizani siku ya leo .

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...