
Naibu
katibu CCM taifa Tanzania bara na mbunge wa jimbo la Iramba magharibi,
Mwigullu Lameck Nchemba akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika
kijiji cha Shelui Iramba magharibi.Pamoja na kutoa taarifa ya maendeleo
yaliyokwishafanyika, Mwigullu alitumia nafasi hiyo kuhimiza maandalizi
ya Kilimo kabla ya mvua kuanza kunyesha.
Mbunge
wa jimbo la Iramba magharibi,Mwigullu Lameck Nchemba (kulia)
akimkabidhi mwenyekiti wa kijiji cha Shelui Saidi Ntunu, moja ya Dawati
kati ya 40 aliotoa msaada kwa shule za msingi Shelui na Ntwike.
Baadhi ya wananchi wa
kijiji cha Shelui wakimsikiliza kwa makini mbunge wao Mwigullu Lameck
Nchemba (hayupo kwenye picha) wakati akizungumza kwenye mkutano wa
hadhara. (Picha na Nathaniel Limu).
. ili kulinda Amani na utulivu wanchi
Na Nathaniel Limu, Shelui
Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi Mwigullu Lameck Nchemba amewaasa vijana wa jimboni humo kujenga utamaduni wa kutafakari kwa undani mambo yanayoenezwa na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa ili kuondoa uwezekano wa kushabikia mambo ambayo yanachangia kuhatarisha amani na utulivu uliopo hivi sasa.
Mwigullu ametoa wito huo hivi karibuni wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Shelui na kuhudhuriwa na umati mkubwa.
Amesema CCM kiliridhia kuanzishwa kwa vyama vingi vya siasa nchini lakini mambo na vitendo vinavyofanywa na baadhi ya vyama vya siasa na hasa CHADEMA ni kinyume na matarajio ya CCM na Watanzania kwa ujumla.
Akifafanua Mwigullu ambaye pia ni Naibu Katibu CCM taifa, amesema mambo yanayofanywa au kuenezwa na CHADEMA mengi yanachangia kupandikiza chuki na mifarakano ambayo imepelekea kuvuruga amani na utulivu.
“Mifano ipo mingi sana inayoonyesha kwamba CHADEMA haipendezwi au imechoka kuwepo kwa amani na utulivu nchini.Hivi karibuni pale Arusha mjini kwenye mkutano wa CHADEMA taifa, Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Arusha ametwagwa ngumi mbele ya Mwenyekiti wa CHADEMA taifa Freeman Mbowe Huo ndio utamaduni wa CHADEMA”,amesema Mwigullu.
Amesema kwa hali hiyo vijana au wakazi wa jimbo la Iramba magharibi endapo watashabikia siasa za CHADEMA zenye lengo la kuhatarisha amani na utulivu hapatakuwepo tena na muendelezo wa maendeleo na badala yake ugomvi na migogoro itatawala.
Katika hatua nyingine Mwigullu amewataka wakazi wa jimbo hilo kufanya maandalizi ya kilimo mapema kabla ya msimu wa mvua haujaanza.
Mbunge huyo amesema maandalizi hayo yaende sambamba na kufuata maelekezo ya wataalam wa kilimo ili kilimo kiwe na tija zaidi.
“Sisi wakazi wa jimbo la Iramba magharibi,tujiwekee malengo ya kujitosheleza kwa chakula kwa mwaka mzima Kujitosheleza huko ni lazima tuwe na maandalizi mapema na tujiwekee malengo katika kilimo chetu”,alifafanua.
Wakati huo huo Mwigullu alitoa msaada wa madawati 40 kwa shule za msingi za Shelui na Ntwike yenye thamani ya zaidi ya shilingi 3.2 milioni.
Na Nathaniel Limu, Shelui
Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi Mwigullu Lameck Nchemba amewaasa vijana wa jimboni humo kujenga utamaduni wa kutafakari kwa undani mambo yanayoenezwa na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa ili kuondoa uwezekano wa kushabikia mambo ambayo yanachangia kuhatarisha amani na utulivu uliopo hivi sasa.
Mwigullu ametoa wito huo hivi karibuni wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Shelui na kuhudhuriwa na umati mkubwa.
Amesema CCM kiliridhia kuanzishwa kwa vyama vingi vya siasa nchini lakini mambo na vitendo vinavyofanywa na baadhi ya vyama vya siasa na hasa CHADEMA ni kinyume na matarajio ya CCM na Watanzania kwa ujumla.
Akifafanua Mwigullu ambaye pia ni Naibu Katibu CCM taifa, amesema mambo yanayofanywa au kuenezwa na CHADEMA mengi yanachangia kupandikiza chuki na mifarakano ambayo imepelekea kuvuruga amani na utulivu.
“Mifano ipo mingi sana inayoonyesha kwamba CHADEMA haipendezwi au imechoka kuwepo kwa amani na utulivu nchini.Hivi karibuni pale Arusha mjini kwenye mkutano wa CHADEMA taifa, Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Arusha ametwagwa ngumi mbele ya Mwenyekiti wa CHADEMA taifa Freeman Mbowe Huo ndio utamaduni wa CHADEMA”,amesema Mwigullu.
Amesema kwa hali hiyo vijana au wakazi wa jimbo la Iramba magharibi endapo watashabikia siasa za CHADEMA zenye lengo la kuhatarisha amani na utulivu hapatakuwepo tena na muendelezo wa maendeleo na badala yake ugomvi na migogoro itatawala.
Katika hatua nyingine Mwigullu amewataka wakazi wa jimbo hilo kufanya maandalizi ya kilimo mapema kabla ya msimu wa mvua haujaanza.
Mbunge huyo amesema maandalizi hayo yaende sambamba na kufuata maelekezo ya wataalam wa kilimo ili kilimo kiwe na tija zaidi.
“Sisi wakazi wa jimbo la Iramba magharibi,tujiwekee malengo ya kujitosheleza kwa chakula kwa mwaka mzima Kujitosheleza huko ni lazima tuwe na maandalizi mapema na tujiwekee malengo katika kilimo chetu”,alifafanua.
Wakati huo huo Mwigullu alitoa msaada wa madawati 40 kwa shule za msingi za Shelui na Ntwike yenye thamani ya zaidi ya shilingi 3.2 milioni.
No comments:
Post a Comment