ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Thursday, December 5, 2013

VIJANA KUWA CHACHU YA MAENDELEO KWA KUJITOLEA NI LAZIMA ILI KUFIKIA MAFANIKIO

IMG_0211
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante OleGabriel akihutubia Vijana (hawapo pichani) katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya kujitolea iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo (jana) IMG_0227Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa (UNDP) Mandisa Mashologu kushoto akimpongeza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni  na Michezo Prof. Elisante OleGabriel mara baada ya kuhutubia katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kujitolea iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo (jana) IMG_0144 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante OleGabriel akikagua moja ya baadhi ya mabanda kuangalia shughuli za kujitolea zinazofanywa  na Vijana
NaGenofeva Matemu (Maelezo)
Vijana watakiwa kuwa na moyo wa kujitolea katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo kwani swala la kujitolea hutoka ndani ya mtu hivyo kuliepushia taifa kuwa na mzigo mkubwa wa vijana wasiojiweza na kupoteza nguvu kazi ya taifa. 
Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel wakati akifungua rasmi Maadhimisho ya Siku ya Kujitolea Duniani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Utalii leo jijini Dar es Salaam. 

Prof. Gabriel amesema kuwa kuna faida nyingi ambazo zinapatikana kutokana na ushiriki wa vijana pamoja na watu wengine katika shughuli za kujitolea ikiwemo ile ya kuchangia kwa kiasi kikubwa katika ongezeko la pato la taifa kupitia shughuli wanazofanya za kujitolea katika jamii. 
Aidha akizungumzia kauli mbiu ya mwaka huu ambayo ni “Young Global Active” ikiwa na maana ya kuwahamasisha vijana kuwa chachu ya maendeleo duniani kote, Prof Gabriel amewataka vijana wa Tanzania kuhakikisha chachu hii inaanzia katika taifa lao kwa kujituma na kutumia fursa mbalimbali zinazojitokeza kushiriki katika shughuli za kujitolea. 
Naye Mkurugenzi msaidizi Kitengo cha Uratibu na Uwezeshaji kwa Vijana Kiuchumi Dr. Kisui Steven Kisui amewataka vijana kujitambua kwa kushiriki katika shughuli za kujitolea zinazoendeshwa kidunia ili waweze kukabiliana na mabadiliko yanayojitokeza katika maisha yao ikiwa ni njia ya kujikwamua kimaendeleo. 
“Kujitolea kunajulikana duniani kote, kunalipa na kumfanya mtu kupata fursa ya kujua vitu vingi kutokana na kupata uzoefu na mawazo katika mitandao mbalimbali ya kujitolea hivyo hatuna budi vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za kujitolea ili tuweze kuepukana na tamaa zisizokua na tija katika maisha yetu” amesema Dr. Kisui. 
Kwa upande wake Meneja Miradi kutoka Million Hours Buguruni Youth Center Bi. Victoria Kululetela kama mmoja wa kijana aliyewahi kujitolea amesema kuwa kwa kujitolea kwake kupitia kampuni tofautitofauti kulimwezesha kupata uwezo wa kusimama mbele za watu na kuzungumza, kuweza kuwa kiongozi mzuri, kuwashawishi vijana wengi zaidi kujitolea katika shughuli za kijamii na kuwashauri wanawake kuanzisha ujasiliamali uliowawezesha kuinua kipato chao. 
Bi. Kululetela amewahamasisha vijana kushiriki katika kazi za kujitolea na kuacha kuangalia zaidi pesa kwani vijana ndilo taifa la leo na ndio viongozi wa badae hivyo wazingatie kujitolea ili waweze kujulikana na kuweza kupata fursa nyinginezo zinazopatikana kwa kujitolea. 
Kujitolea kuligundulika kama sehemu muhimu ya maendeleo miaka kumi iliyopita, mwaka 2001 pale wanachama 126 walipopitisha azimio mwishoni mwa mwaka wa kimataifa wa wajitoleaji (IVY). Mwaka huu maadhimisho ya siku ya kujitolea duniani yamefanyika kuanzia tarehe 25 novemba mpaka tarehe 05 desemba yakiwa na lengo la kuwainua vijana kuwa chachu ya maendeleo. 

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...