ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Thursday, May 15, 2014

WACHEZAJI WA SEVILLA WANYONYANA NDIMI KUSHEREHEKEA TAJI LA EUROPA LEAGUE


SEVILLA ya Hispania imetwaa ubingwa wa Europa League baada ya kuifunga Benfica ya Ureno kwa penalti 4-2 kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 120.
Mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Juventus, mjini Torino, Italia ulikuwa wa kawaida na timu zote zilicheza kwa tahadhari, hali iliyosababisha hata mashambulizi yawe machache
Bacca, M’Bia, Coke na Gameiro ndiyo walifunga penalti za Sevilla, wakati wa Cardozo na Rodrigo walikosa za Benfica, huku Lima na Luisao wakifunga.
Sifa zimuendee kipa Mreno wa Sevilla Antonio Alberto Bastos Pimparel aliyewazuilia ndugu zake leo na kucheza penalti moja ya Rodrigo, wakati ya Cardozo ilikwenda nje.  Ushindi wa Sevilla unamaanisha mataji yote ya klabu ya UEFA msimu huu yamebaki Hispania, kwani Atletico Madrid na Real Madrid nazo zitakutana katika Fainali ya Ligi ya Mabingwa baadaye mwezi huu nchini Ureno. 

Vikosi vilikuwa, Sevilla:
 Beto, Coke, Pareja, Fazio, Moreno, Mbia, Carrico, Reyes/Marin dk78/Gameiro dk104, Rakitic, Vitolo/Diogo Figueiras dk110 na Bacca. Benfica:
 Oblak, Maxi Pereira, Luisao, Garay, Siqueira/Cardozo dk99, Ruben Amorim, Gomes, Gaitan/Ivan Calvaleiro dk119, Sulejmani/Andre Almeida dk25, Lima na Rodrigo.

Tukio lingine lililo make head line jana ni KIUNGO Ivan Rakitic alikuwa nyota usiku wa jana wakati Seville ikiifunga Benfica kwa penalti na kutwaa taji la Europa League mjini Turin.
Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Croatia alicheza soka ya kiwango cha nyota wa mchezo na kisha akamalizia kwa kunyonyana mdimi na beki wa zamani wa Reading, Daniel Carrico.
Rakitic amekuwa mmoja wa viungo bora barani Ulaya kwa sasa  kiasi cha timu kibao barani humo sass kuanza kuisaka huduma yake.



Silverware: Rakitic poses with the Europa League trophy after Sevilla beat Benfica on penalties
Taji: Rakitic akiwa amepozi na taji Europa League usiku wa kuamkia leo baada ya Sevilla kuifunga Benfica kwa penalti.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...