ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Saturday, September 13, 2014

Fred Mpendazoe kumrithi Arfi Umakamu Chadema Bar?


Mpendazoe 037[2]
Aliyekuwa mgombea wa ubunge katika Jimbo la Segerea kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Fred Mpendazoe.
Na Mwandishi wetu
Aliyekuwa mgombea wa ubunge katika Jimbo la Segerea kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Fred Mpendazoe amejitokeza kuwania nafasi ya Makamu mwenyekiti wa chama hicho.
Mpendazoe ambaye amewahi kuwa Mbunge wa Kishapu kupitia CCM kabla ya kujiuzulu wadhifa huo na kujiunga na Chadema  ametangaza msimamo wake akisema kuwa atasimamia ajenda zifuatazo kuhakikisha Chadema inachukua dola 2015
Mkakati wa kwanza  amesema akichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti ataimarisha Chadema kama taasisi, akisema kuwa mfumo uliopo sasa haujawa imara hasa sehemu za msingi na matawi.
Alifafanua kuwa  wanananchi wengi hujitokeza kwenye mikutano ya hadharal akini inakuwa  vigumu kuwafuata ili kuwapatia elimu ya uraia
Hivyo akiwa Makamu Mwenyekiti atashawishi vikao vya maamuzi kama kamati kuu kutenga rasilimali za kutosha kwenda kuimarisha misingi, matawi na ofisi za majimbo na mikoa.
Mkakati wa pili ni kwamba atatumia uzoefu wake wa siku nyingi aliofanya kazi serikalini kusaidia Chadema kupata wanachama katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu 2015, kwani ana uhakika ana ushawishi mkubwa kwenye jamii ya wtanzania.
Amesisitiza kuwa “Chama ni wanachama, na chama ni vikao. Na Uimara wa Chama chochote cha siasa unatokana na uimara wa Mabaraza yake ya Vijana, wanawake na wazee. Ninao ushawishi wa kuifanya Chadema ikubalike na kuungwa mkono na kupata wanachama nchini kote ndani ya Chama nitashawishi  mabaraza yapewe vitendea kazi ili yaimarike.
Ndani ya chama nitaimarisha demokrasia, maoni na mtazamo tofauti ijadiliwe hadi maafikiano yakubaliwe. Nitasimamia dhana ya Papa na Mkulima ni bora kuliko Papa peke yake.
Nitasimamia kauli mbiu ya Martin Luther King inayosema “Binadamu yeyote kama hajagundua jambo lolote ambalo hayuko tayari kufikwa nalo hafai kuishi.
Mimi sitaki kuwa miongoni mwa wafu wanaotembea, nimeamua kuwapigania watanzania masikini, wanyonge wanaonyanyaswa na utawala dhalimu wa CCM.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...