Baadhi ya silaha zilizokamatwa na jeshi la polisi.
Kamanda Suleiman Kova akionyesha silaha zilizokamatwa kwa wanahabari (hawapo pichani).
Baadhi ya wanahabari wakimsikiliza Kova.
JESHI la ×Polisi Kanda Maalum ya Dar es ×Salaam
linamshikilia mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Gunner Meena (40)
mkazi wa Kinyerezi, Segerea, Dar es Salaam, kwa tuhuma za
kujifanya mtumishi wa ×Idara ya Usalama wa Taifa .
Tukio la mwisho lililomfanya akamatwe ni pale alipomtishia mfanyabiashara mwenye asili ya ×Kisomali aitwaye Abdi Dalmar, ili ampe Tshs 25,000,000/= ama sivyo angechukua hatua chini ya ×Sheria ya Usalama wa Taifa.
Aidha
jeshi hilo katika kuendesha oparesheni zake za kutokomeza ujambazi wa
kutumia silaha limefanikiwa kukamata bastola nne na shot-gun moja wiki
hii.
No comments:
Post a Comment