Moja
kati ya majeneza yaliyohifadhiwa miili ya marehemu yakitolewa ndani ya
chumba hicho.Chanzo cha kuaminika kimeeleza kuwa wawili hao ambao
walikuwa wakifanya kazi katika baa iitwayo Mashua iliyo ndani ya
Slipway, huku mwanamke, aliyetajwa kwa jina la Hotsan, akiwa ndiye
Meneja, walikutwa chumbani kwao wakiwa wamefariki baada ya kutoonekana
kazini tokea Jumanne, siku ambayo Watanzania walikuwa wakikumbuka miaka
15 baada ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.
WAZUNGU wawili ambao ni mume na mke wanaodaiwa kuwa ni raia wa Afrika
Kusini, wamekutwa wamekufa chumbani kwao katika nyumba waliyokuwa
wakiishi maeneo ya Slipway, Masaki jijini Dar es Salaam Jumatano hii.
Inadaiwa kuwa baada ya kutotokea kazini katika muda wa kawaida,
wafanyakazi wenzao walijaribu kupiga simu zao za mikononi, lakini zote
zilikuwa zikiita pasipo kupokelewa karibu mchana kutwa na hivyo kuwapa
maswali mengi yasiyo na majibu.
Siku iliyofuata, inadaiwa kuwa wafanyakazi wenzao walipojaribu tena kupiga namba hizo, simu zote mbili hazikupatikana
Jeneza lingine likitolewa ndani ya chumba hicho. Awali, walihisi
huenda wenzao wameamua kuacha kazi baada ya kupata sehemu nyingine,
lakini baadaye wakafikia uamuzi wa kuwafuatilia nyumbani kwao ili kujua
kilichotokea.
Walipofika, walikuta milango ikiwa imefungwa kwa ndani, kitu
kilichowafanya waamini kuwa walikuwa ndani. Kwa kushirikiana na
majirani, wafanyakazi hao waliamua kuvunja mlango wa chumba wanacholala
wanandoa hao na kuwakuta wakiwa kitandani wamelala, kila mmoja akiwa
amegeukia upande wake.
Baada ya kuona tukio hilo la kushtusha, waliamua kuwaita Polisi ambao
walipofika na kuiona miili hiyo, waliamua kuwaita wenzao wa kitengo
maalum cha uchunguzi (Crime Investigation) ambao baada ya kufika,
waliwataka raia na majirani waliokusanyika hapo kukaa mbali ili
kuwapisha kufanya uchunguzi.
Kamanda Suleiman Kova. Askari hao walikaa na miili ya marehemu kwa
zaidi ya saa tatu wakiwafanyia uchunguzi na baada ya kukamilika kwa
zoezi hili, miili hiyo ilichukuliwa kupelekwa hospitalini Muhimbili.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura alithibitisha
kutokea kwa tukio hilo na kuwataja marehemu kuwa ni Roxxana Hilari na
Hainess Hilton William na kwamba uchunguzi zaidi juu ya kilichowaua
unaendelea.
No comments:
Post a Comment