Makamu wa Rais wa
Afrika Kusini, Mhe. Matamela Cyril Ramaphosa akiteremka katika ndege
mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius
Nyerere Jijini Dar es Salaam. Mhe. Ramaphosa yupo nchini kwa ziara ya
kikazi ya siku moja ambapo pamoja na mambo mengine atazungumza na Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais, Mahusiano , Mhe. Stephen Wasira kwa pamoja na Naibu Waziri wa
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dkt. Mahadhi Juma Maalim
(Mb), na Bi. Zuhura Bundala, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika
katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati wa
mapokezi ya Makamu wa Rais wa Afrika Kusini.
Mhe. Ramaphosa akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika mara baada ya kuwasili.
Mhe. Ramaphosa akisalimiana na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Talha Mohammed
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Ikulu
Makamu wa Rais wa Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa Matamela alipofika
Ikulu kwa mazungumzo.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Makamu
wa Rais wa Afrika Kusini Mhe. Ramaphosa.
Waziri wa Mambo ya
Nje na Ushirikino wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) kwa pamoja na
Mhe. Wasira wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Rais na Makamu wa Rais
wa Afrika Kusini (hawapo pichani)
Mazungumzo yakiendelea. Kulia ni Mhe. Radhia Msuya, Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini
Picha ya pamoja mara baada ya kumaliza mazungumzo.Picha na Reginald Philip
No comments:
Post a Comment