Baba Askofu Methodius
KilainiDar es Salaam. Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Methodius
Kilaini amekiri kupokea Sh80.5 milioni kutoka kwa Mkurugenzi wa VIP
Engeering, James Rugemalira akisema si mara yake kwa kwanza kupokea
fedha kutoka kwa mfanyabiashara huyo kwa kuwa mara nyingi huwa
anachangia kwa uwazi miradi ya jamii.
Askofu huyo alikuwa
akizungumzia Ripoti ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC),
iliyosomwa bungeni juzi ikimtaja kuwa ni miongoni mwa viongozi wa dini
na watu wengine waliopokea mabilioni kutoka katika akaunti ya escrow.
Katika ripoti hiyo,
Zitto aliwataja viongozi wengine wa dini walioingiziwa fedha katika
Benki ya Mkombozi inayomilikiwa na Kanisa Katoliki kuwa ni Askofu
Eusebius Nzigirwa (Sh40.4 milioni) na Padri Alphonce Twimanye Simon
(Sh40.4 milioni).
Akizungumza kwa simu jana, Askofu Kilaini alisema Rugemalira
hupendelea kuchangia kwa uwazi miradi ya kijamii na si yeye peke yake aliyempatia mchango, bali kuna watu wengine wengi ambao wameshampatia na kazi yake ni kuipokea na kuifikisha sehemu husika.
hupendelea kuchangia kwa uwazi miradi ya kijamii na si yeye peke yake aliyempatia mchango, bali kuna watu wengine wengi ambao wameshampatia na kazi yake ni kuipokea na kuifikisha sehemu husika.
Hata hivyo, kabla hajafafanua zaidi hoja yake, simu ilikatika na baadaye hakupatikana tena.
Hata hivyo, jana
askofu huyo alinukuliwa na Gazeti la Mawio toleo la jana akisema fedha
alizozipokea kutoka kwa Rugemalira ni kwa ajili ya miradi mbalimbali
inayoendeshwa na Kanisa Katoliki.
“Ndiyo nimepokea
fedha kutoka kwa James na hii siyo mara ya kwanza, kwani mara nyingi
amekuwa akichangia miradi mbalimbali ya kijamii,” alisema Askofu
Kilaini.
No comments:
Post a Comment