ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Wednesday, February 4, 2015

Majeshi ya Chad yaingia Nigeria


Magari ya jeshi la Chad yakiegesha katika mji wa  Fotokol, kwenye mpaka wa Cameroon, yakielekea katika mji wa Gamboru, nchini Nigeria, Jumapili Februari 1.
Vita dhidi ya Boko Haram vimeshika kasi tangu Chad ilipopeleka kikosi cha wanajeshi wake kwenye mpaka wa Cameroon, katika mji wa Fotokol. Jumanne mchana wiki hii, askari wa Chad wameingia katika mji wa Gamboru, nchini Nigeria.
Wanajeshi wa ardhini na magari ya kijeshi ya jeshi la Chad, ambayo yalikua katika mji wa Fotokol, nchini Cameroon, wamevuka mpaka leo Jumanne mchana na kupiga kambi upande wa pili wa daraja, katika mji wa Gamboru, nchini Nigeria, uongozi wa jeshi la Chad umethibitisha leo Jumanne Februari 3.
Operesheni hizo za ardhini zimefuatiwa na mashambulizi ya angani, ambayo yamedumu takribani saa moja. Mji wa Gamboru, umeshuhudia mashambulizi ya majeshi ya Chad na Cameroon kwa muda wa siku tatu mfululizo.
Boko Haram ilikua iliuteka mji huo katika mashambulizi makali iliyoendesha mwanzoni mwa mwezi Januari. Wakati huo wapiganaji wa Boko Haram walishambulia ngome za wanajeshi wa Chad. Kwa kujibu mashambulizi hayo, wanajeshi wa Chad walijaribu Jumamosi Januari 31, kuingia katika mji wa Gamboru, kabla ya kuanza mashambulizi dhidi ya Boko Haram.
Jumatatu wiki hii, viongozi wa Nigeria walithibitisha kwamba mji wa Gamboru uko chini ya udhibiti wa majeshi ya Chad, jambo ambalo sio kweli, kufuatia mapigano ya leo Jumanne asubuhi. Jumanne mchana, takribani wanajeshi 2000 wa Chad waliokua katika mji wa Fotokol, walionekana wakivuka mpaka na kuingia Nigeria

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...