| Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) ambao umefunguliwa rasmi leo tarehe 30 Januari, 2014 mjini Addis Ababa, Ethiopia. |
| Rais Mpya wa Madagascar, Mhe. Henry Rajaonarimampianina akitoa hotuba yake ya shukrani kwa nchi za Afrika kwa michango yao iliyopelekea uchaguzi wa amani na demokrasia nchini Madagascar na pia kwa Madagascar kurejea AU. |
| Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. hailemariam Dessalegn akitoa hotuba kama Mwenyekiti wa AU anayemaliza muda wake kabla ya kukabidhi nafasi hiyo kwa Rais wa Mauritania, Mhe. Mohamed Ould Abdel Aziz. |
| Rais wa Mauritania, Mhe. Mohamed Ould Abdel Aziz akitoa hotuba kama Mwenyekiti Mpya wa Umoja wa Afrika kwa kipindi cha mwaka mmoja hadi Januari 2015. |
| Picha ya Pamoja ya Viongozi wa AU. |
| Mhe. Membe akiongozana na Rais wa Zimbabwe, Mhe. Robert Mugabe mara baada ya hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa AU |
| Mhe. Membe akiteta jambo na Rais wa Afrika Kusini, Mhe. Jacob Zuma nje ya Ukumbi wa Mikutano wa AU.
Kiswahili chazidi kupaa Umoja wa Afrika
Na Mwandishi wetu, Addis Ababa
Umoja
wa Afrika umeitaja Lugha ya Kiswahili kuwa ndiyo lugha kubwa na rasmi
Afrika na ndio Lugha inayofundishwa zaidi katika Vyuo Vikuu mbalimbali
duniani kutoka Afrika.
|