ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Sunday, February 16, 2014

Barcelona waitandika Rayo Vallecano Goli 6 Bila


Lionel Messi amefunga mara mbili wakati klabu yake ya Barcelona ikijiandaa na mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya jumanne ijayo dhidi ya Manchester City kwa kuichapa bila huruma Rayo Vallecano mabao 6-0 na kujikita kileleni mwa msimamo wa La Liga.
Mlinzi wa kushoto Adriano alifunga bao la ufunguzi kabla Messi hajapiga bao la pili.


Mabao mengine yamefungwa na Alexis Sanchez, Pedro, Messi na Neymar.
Katika mchezo mwingine wa La Liga, Atletico Madrid imeichapa Real Valladolid mabao 3-0. Mabao ya washindi yakifungwa na kiungo Raul Garcia, Diego Costa na mlinzi Diego Godin.
Nayo Levante imeichapa Almeria 1-0 na Villarreal imekubali kipigo cha 2-0 kutoka kwa Celta de Vigo

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...