ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Monday, February 17, 2014

Wajumbe wa Bunge la Katiba kulipwa sh. 300,000 kwa siku na siyo sh. 700,000/= kama ilivyodaiwa hapo awali


2
Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Thomas Kashillilah (katikati ) akiongea na Waandishi wa Habari.
Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Thomas Kashillilah, amewaambia waandishi wa habari kuwa  Bunge Maalumu la Katiba litazinduliwa rasmi Februari 26, 2014 huku kila mjumbe akilipwa posho ya shilingi laki tatu na siyo shilingi laki saba kama ilivyochapishwa katika baadhi ya vyombo vya habari.
“Sisi tumesikia kuwa Wabunge wa Bunge la Katiba wanalipwa 700,000 na wala hatujui hili limetoka wapi, kwanza mamlaka ya kuidhibisha posho ni la Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania na hajaidhinisha Sh. 700,000.
Alisema Wajumbe watalipwa posho ya kawaida ya Serikali ya siku (hakuitaja), lakini alisema kutawakuwa na kodi maalumu ambayo itahusisha posho ya kikao, usafiri, malipo kwa madereva na mengineyo. Hivyo posho ya kawaida itakuwa Sh 80,000/=

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...