ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Friday, March 6, 2015

Kufichua mafisadi salama ya CCM- Abdulrahman Kinana

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa Jimbo la Kongwa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Mkoka,wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma ikiwa sehemu ya muendelezo wa ziara zake za kukagua utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya CCM mwaka 2010.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Mkoka wilayani Kongwa na kuwaambia moja ya sifa muhimu na ya kipekee kwa kiongozi anayefaa kuongoza wananchi ni Uadilifu.
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma Mheshimiwa Adam Kimbisa akihutubia wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa hadhara ambao Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alikuwa mgeni wa Heshima, Kimbisa aliwaambia wana CCM kuwa Dodoma itakuwa mfano katika kutenda haki.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Mkoka wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma ambapo aliwaambia wananchi hao CCM ni Chama pekee chenye kujali Watanzania kinachosimamia na kuitunza amani iliyokuwepo
 

Mpwapwa.Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana amesema kitu kitakachokiokoa chama hicho ni wanachama kutowafumbia macho wezi na mafisadi akisisitiza kuwa kulindana na upole kutakiangamiza chama hicho kikongwe.
Kinana amesema hayo wakati CCM ikizidi kuchafuliwa na kashfa za ufisadi ambazo zimekuwa zikiwakabili makada wake ambao mara kadhaa wamelazimika kuachia ngazi baada ya Bunge kukomaa kutaka hatua zichukuliwe.
Tayari makada wa CCM wameshalazimika kuwajibika katika kashfa za uchotwaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow ambako zaidi ya Sh306 bilioni zilichotwa, kashfa ya Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), kashfa iliyoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kashfa ya rada na nyingine kwenye sekta ya utalii.
Tayari makada wa CCM wameshalazimika kuwajibika katika kashfa za uchotwaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow ambako zaidi ya Sh306 bilioni zilichotwa, kashfa ya Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), kashfa iliyoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kashfa ya rada na nyingine kwenye sekta ya utalii.
Kinana, ambaye amekuwa akishambulia viongozi wa Serikali kwenye ziara zake, alitoa agizo hilo juzi wakati alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara kwenye Viwanja vya Kibakwe wilayani Mpwapwa ambako alisema kufanya hivyo ndiyo salama ya CCM.
“Tatizo lenu (wanachama wa CCM) mnakuwa wapole na mnajenga tabia ya kulindana. Kwa njia hiyo hamtaweza kukisaidia chama chenu. Mtu akikosea hakuna bahati mbaya, ondoa huyo na apelekwe jela mara moja ili kazi nyingine zisonge,” alisema Kinana ambaye hata hivyo hujiepusha kuzungumzia kashfa hizo kubwa kwenye mikutano yake.
Kwa upande mwingine alisema kuwa ndani ya CCM kuna baadhi ya wanachama wezi ambao alidai hawajai kiganja kati ya wanaCCM 7 milioni, lakini wamesababisha wanaCCM kudharauliwa na kuwakosesha raha maskini wengi walioko vijijini ambao alisema wanaendelea kutukanwa kuwa ni mafisadi jambo ambalo siyo kweli.
Huku akishangiliwa na umati mkubwa uliohudhuria mkutano huo, alisema dhambi mbaya kwa sasa ni ile ya kufanya kazi kwa mazoea na kulindana kwa kisingizio cha utawala bora wakati wezi wanaiba bila ya kuangalia masuala ya utawala bora.
Kauli ya Kinana huenda ikawapa nguvu baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wakisimama kidete kwa ajili ya kupinga ufisadi, lakini mara kadhaa wakiwa bungeni hushindwa katika mapambano yao kutokana na misimamo ya chama.
Kinana alisema suala la wanachama wa CCM kuimba “iyena iyena” huku wakiwa wapole huu siyo wakati wake badala yake wabadilike na kukemea maovu na mambo yanayokwenda kinyume na chama chao.
 “Nasema kwa wanachama wa CCM nchi nzima, mpango wa kuhamisha mtu kutoka eneo moja na kupelekwa sehemu nyingine huo usiwepo, mtu akituhumiwa lazima aachie ngazi akisubiri uchunguzi,” alisema na kuongeza.
“Wakati wa kuiba wezi hawafuati utawala bora, lakini wanapotakiwa kuondoka ndipo masuala ya utawala bora yanapoanza kusimama, naona suala la utawala bora litazamwe upya maana wengine hawafanyi kama tulivyowatuma.”

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...