Andrew Chenge na aliyekuwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ambao wametajwa
kutaka kuwania nafasi ya uenyekiti wa Bunge la Katiba wakipeana mikono
siku za hivi karibuni.
Na Kizitto Noya, Mwananchi
- Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa makundi hayo ni yale yanayomsaidia aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Andrew Chenge na aliyekuwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ambao wametajwa kutaka kuwania nafasi hiyo.
Dodoma. Kadiri siku
zinavyosogelea uchaguzi wa Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, ndivyo
mpasuko ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) unavyozidi, kutokana na
kuwapo kwa makundi mawili yanayojipanga kusimamisha wagombea na ambayo
yameanza kuendesha kampeni kuchafuana.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa makundi
hayo ni yale yanayomsaidia aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali,
Andrew Chenge na aliyekuwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta, ambao wametajwa
kutaka kuwania nafasi hiyo.