London, England. Milango ipo wazi kwa
klabu kubwa za Ligi Kuu England kumsajili kiungo wa Bayern Munich, Toni
Kroos ambaye mazungumzo ya mkataba wake mpya na klabu yake yamevunjika.
Kroos, amekuwa akifuatiliwa kwa karibu na Manchester United hasa wakati wa dirisha dogo la usajili ambalo lilifungwa Januari 31.
Kiungo huyo ambaye thamani yake ni
Pauni 25 aliingia matatani wiki iliyopita baada ya kutolewa katika
mchezo wa Ligi Kuu ya Ujerumani dhidi ya Stuttgart, jambo ambalo
lilimchukiza.
Kitendo hicho kilimchefua kocha wake, Pep Guardiola ambaye ameamua kumwondoa katika kikosi chake.