ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI
Showing posts with label simba. Show all posts
Showing posts with label simba. Show all posts

Sunday, December 14, 2014

Timu ya Simba ilivyoibamiza Yanga jana.



 Emmanue Okwi akiomba dua wakati akiingia uwanjani.
 Kocha wa Simba, Patrick Phir akisalimiana na kocha wa Yanga, Marcio Maximo kabla ya mchezo. (Picha zote na
Francis Dande)
 Mgeni rasmi akisalimiana na wachezaji wa Yanga.
 Mgeni rasmi akisalimiana na wachezaji wa Simba.
Kikosi cha Yanga.
Kikosi cha Simba.
Kocha wa Yanga akitafakari.
Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi akiwa amenyanyua juu Kombe la Ubingwa wa mechi ya Nani Mtani Jembe msimu wa pili uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Simba imeshinda 2-0.

 Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Mchezo, Dk. Fenella Mukangala akimkabidhi nahodha wa Simba, Emmanuel Okwi Kombe la Ubingwa wa mechi ya Nani Mtani Jembe.

Wachezaji wa Simba wakishangilia ushindi wa timu yao.


 Umati wa mashabiki wa Yanga.

 Umati wa mashabiki wa Simba.
Mashabiki wa Simba wakiwa wamebeba mfano wa jeneza kuwakejeli watani zao.

 Beki wa Yanga, Nadir Haroub 'Canavaro'

 Beki wa Yanga, Kelvin Yondan akimiliki mpira.

 Mwamuzi wa mchezo akimuonyesha kadi ya njano mshambuliaji wa Simba, Simon Serunkuma.

 Kpah Sherman akiokoa moja ya hatari langoni mwake huku Elius Maguri akimzonga.

 Mshambuliaji wa Simba Emmanule Maguri akichuana na beki wa Yanga, Nadir Haroub.

Wachezaji wa Simba wakishangilia bao lao la kwanza.

 Hassan Isihaka (kushoto) ana Ramadhani Singano 'messi' wakishangilia bao la kwanza la timu yao.

Beki wa Yanga, Oscar Joshua akimtoka Elius Maguri wa Simba.

Shabiki wa Yanga akipata msaada baada ya kuzimia jukwaani.

 Mashabiki wa Simba wakiwa na bango lenye idadi ya mabao waliyowahi kufungwa Yanga.

Leo ni 2-0.....

Burudani zikitolewa uwanjani.

 Mashabiki wakitolewa uwanjani baada ya kuzimia.
 Hali ilikuwa ngumu kwa mashabiki mpaka baadhi yao kuzimia.
Huduma ya kwanza kwa waliozimia ikitolewa.

 Beki wa Yanga, Kpah Sherman akichuana na beki wa Simba, Hassan Isihaka.

 Danny Mrwanda akiwa ameshika kichwa baada ya kukosa bao la wazi.
Ivo Mapunda akiokoa moja ya hatari langoni mwake.

 Simon Msuva akichuana na Issa Rashid.

Ivo Mapunda (katikati) akishangilia ushindi na wenzake.
Wachezaji wa Yanga wakiwa na huzuni baada ya kumalizika kwa mchezo.
Yanga wakiwa vichwa chini.

 Medali za washindi.

Thursday, July 17, 2014

NAIBU WAZIRI WA WIZARA YA HABARI,VIJANA,NA MICHEZO AZINDUA RASMI KITABU CHA "HISTORIA YA KLABU YA SIMBA"KILICHOANDIKWA NA MWINA KADUGUDA

 Mwina Kaduguda Mtunzi wa kitabu cha "HISTORIA YA SIMBA" akielezea kwa kina Magumu gani amepitia wakati anaanza kuandaa kitabu hicho,Wa kwanza Kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Juma Nkamia na Katikati ni Mkurugenzi wa Mkuki na Nyota Bwana Mkuki Bgoya ambao ndio wachapishaji wa kitabu hicho.Akielezea kwa ufupi Mwina Kaduguda amesema kwamba Dhumuni kubwa la Kutunga kitabu hicho ni kutaka kutunza historia ya soka ya Timu hiyo isipoteee ili iweze kusomwa kizazi na kizazi.



 Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Juma Nkamia Akijiandaa kukata utepe ili kuweza kuzindua rasmi kitabu hicho cha historia ya Simba,Wanaoshuhudia kulia ni mtunzi wa kitabu hicho Mwina Kaduguda akifuatiwa na Bwana Mkuki Bgoya mkurugenzi wa Mkuki na Nyota Ambao ndio wachapishaji wa kitabu hicho
Mkurugenzi wa Mkuki na Nyota Bwana Mkuki Bgoya  Akielezea namna walivyochapa kitabu hicho na ubora wake .
 Mjumbe wa kamati ya Utendaji Klabu ya Simba Bwana Collin Frisch akiongea kwa niaba ya Rais wa Simba,ambapo amempongeza sana Mwina Kaduguda na kusema ameiweka Klabu ya Simba kwenye Kumbukumbu muhimu sana kwenye soka la Tanzania hivyo inatakiwa aungwe mkono kwa nguvu zote.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Juma Nkamia akitoa neno kumpongeza Mwina Kaduguda  kwa kufikiria mbali sana kwa kuweka soka la Tanzania kwenye maandishi namna klabu ya simba ilivyoanza,Akaongeza kuwa Klabu za soka Tanzania zinatakiwa kuwa na watu kama Mwina Kaduguda ili kuleta maendeleo ya soka.Naibu waziri pia akasisitiza ni wakati wa kila mwanachama kujituma kwa bidii na kuacha kukaaa kwenye korido za Klabu na kupiga Zoga.

 
Mwina kaduguda Mtunzi wa Kitabu cha "HISTORIA YA SIMBA" Akimkabidhi  Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Juma Nkamia Zawadi ya Kitabu ambayo ameomba apelekewe Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
 Mwina kaduguda Mtunzi wa Kitabu cha "HISTORIA YA SIMBA" Akimkabidhi  Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Juma Nkamia Zawadi yake ya Kitabu.
 Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Klabu ya Simba Collin Frisch akiwa na Mtunzi wa kitabu cha Historia ya Simba Mwina Kaduguda kwenye uzinduzi Rasmi wa kitabu hicho kwenye ukumbi wa Klabu ya Simba
 Wageni waalikwa waliokuja Kushuhudia Uzinduzi wa Kitabu cha "HISTORIA YA SIMBA" Kutoka kulia ni Fredrick Mwakalebela,Said Tulliy(Mjumbe wa kamati ya Utendaji),Hassan Dalali(mwenyekiti Mstaafu) na Mtunzi wa kitabu Hicho Mwina Kaduguda
 Wapenzi,wanachama wa Simba Pamoja na Vyombo vya habari waliohudhuria Uzinduzi wa Kitabu cha "HISTORIA YA SIMBA" wakifuatilia kwa makini Uzinduzi huo
Hizo ni kopi za Kitabu cha "HISTORIA YA SIMBA" kilichozinduliwa leo na Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Juma Nkamia

Tuesday, November 19, 2013

HUYU NDIYE MWENYEKITI MPYA WA SIMMBA

RageSimbaKamati ya  utendaji ya klabu ya Simba iliyokutana jana usiku imempiga stop Ismail Aden Rage kuendelea na ubosi katika klabu ya Simba na kulibadilisha benchi la ufundi isipokuwa nafasi ya meneja Madaktari wa timu ambapo pia kwa sasa wanamtarajia ZDRAVOK LOGARUSIC kutoka Croatia.
 Akizungumza kwa niaba ya kamati ya utendaji, mjumbe wa kamati ya utendaji Joseph Itangare amesema wamemsimamisha mwenyekiti kutokana na kufanya maamuzi yake binafsi bila kushirikisha kamati ya utendaji ikiwemo kutoitisha vikao vya kamati ya utendaji kwa mujibu wa Ibara ya 31 (1)ya katiba ya simba.
Kingine alichosema Itangare ni ‘vilevile mwenyekiti huyo amesaini mkataba wa kukiuuza kipindi cha Simba tv bila kushirikisha kamati ya utendaji’
Mzee Kinesi
Hii picha hapa juu ni Mzee Kinesi ambae namkariri akisema ‘kwa sasa lazima twende kikatiba, Mwenyekiti kama hayupo ngazi inayofatia inapanda juu na tunachagua Mjumbe mwingine ili kukaa kwenye nafasi iliyobakia, kwa muda huu wa matayarisho ya mkutano mkuu ujao mimi nitakaimu kama Mwenyekiti wa Simba na Swed atakaimu kama makamu Mwenyekiti’ (picha kutoka kwa salehjembe.blogspot.com)
Kwenye sentensi nyingine, Kinesi amesema ‘Mwenyekiti tumemsimamisha lakini tusubiri maamuzi ya mkutano mkuu ambao utafanyika kwa ajili ya marekebisho ya katiba, kuna mengine yamekiukwa hivyo yatawasilishwa kwenye mkutano mkuu tarehe 1 December’
‘Kutokana na timu yetu kutofanya vizuri, tumeamua kwamba benchi la ufundi tulifumue ili tulijenge upya, sasa litaongozwa na kocha aliekua na Gor MahiaZDRAVOK LOGARUSIC amekubali kuja na ataanza mazoezi tarehe 2 December na kwa pamoja tumekubaliana ndie atakua kocha mkuu, pia tumekubaliana Matola ndio awe msaidizi wake kwa muda, hatumuondoi Simba B moja kwa moja kuhofia kutetereka’
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...