ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Sunday, December 9, 2012

Kansa ya Hogo Chaves yarudi tna kwa kazi.




Hugo Chavez akiwa hana nywele baada ya kutumia dawa za chemotherapy kwa ajili ya kutibu kanser
 
Chavez akiongea na waandishi wa habari  akiwa na Nicolas Maduro pembeni
  
 
Chavez akiwa na Castro

 
Nicolas Maduro mrithi wa Hogo Chavez 

 
 
Maduro aliyekuwa dereva wa basi sasa anatarajiwa kuwa rais wa Venezuela ikiwa Hogo Chaves atashindwa kutokana na ugonjwa wa Kansa unaomsumbua


Rais wa Venezuela Hogo Chaves amewaambia wananchi wa  Venezuela jana kuwa, ugonjwa uliokuwa unamsumbua wa kansa umerejea tena. Chaves ambaye alienda Cuma kwa siku kumi kwa ajili ya kuchunguza tena afya yake amerudi jijini Caracas na kuweka wazi zaidi kwa mara ya kwanza kuhusu kansa ambayo awali ilikuwa imedhibitiwa na madaktari wa Cuba.
Caves mwenye umri wa miaka 58 sasa amekuwa kiongozi mwenye msimamo mkali kuhusu sera za mafuta na sera za mambo ya nje, amekuwa akipingana waziwazi na maamuzi yanayofanywa na mataifa ya Magharibi na Marekani.
Chavez ambaye amechaguliwa tena kuiongoza Venezuela kwa kipindi kingine cha miaka 6 anatarajiwa kuapishwa rasmi tarehe 10 januari lakini duru za kiuchunguzi zinaonyesha kuwa huenda kuapishwa kwake kukaahirishwa kutokana na ugnjwa wake na kwa kuwa atakuwa anafanyiwa matibabu huko Cuba.
Kwa mara ya kwanza Chaves ameweka wazi kwamba, kama hali yake ya afya itaendelea kuwa mbaya kiasi cha kushindwa kuiongoza Venezuela basi achaguliwe makamu wake wa rais Bwana Nicolas Maduro. Maduro ambaye awali alikuwa dereva wa mabasi, alikuwa msemaji mahiri sana wa Chaves kabla ya kuteuliwa kuwa waziri wa mambo ya nje kwa kipindi kirefu na hivi karibuni akateuliwa kuwa makamu wa rais.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...