ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Tuesday, December 4, 2012

Profesa Muhongo azungumza na Chama cha Wafanyabiashara ya Madini kuhusiana na Masuala nyeti kuboresha Sekta hiyo.


Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Profesa Sospeter Muhongo akimsikiliza Mwenyekiti wa Chama Cha Wafanyabiashara ya Madini (TAMIDA), Bw. S. Sammy Mollel walipokutana katika makao makuu ya Wizara ya Nishati na Madini ili kujadili masuala mbalimbali yanayohusiana na biashara ya madini nchini ikiwa ni pamoja na ufungaji na usafirishaji wa vifurushi na mizigo ya madini, ongezeko la kodi ya thamani ya asilimia 18 ya madini, bei elekezi ya uuzaji wa madini inayotolewa na TANSORT, ada za leseni za wafanyabiashara na uombaji wa kibali maalumu kwa watalii wanaonunua madini ya vito kwenye maduka ya vito.

Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Profesa Sospeter Muhongo akitoa ufafanuzi wa baadhi ya hoja zilizokuwa zikijadiliwa na Wafanyabiashara wa Madini nchini ambapo aliunda kamati maalumu ambayo itahusika na upangaji wa bei elekezi ya madini. Kamati hiyo itahusisha wajumbe mbalimbali kutoka wizarani, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wawakilishi kutoka Chama cha Wafanyabishara ya Madini nchini (TAMIDA). Kamati hiyo itaongozwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthamini wa Almasi na Vito Tanzania. (TANSORT)

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...