ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Friday, December 28, 2012

Sakata la mvamizi aliyeungua moto hadi kufa ndani ya nyumba ya mwanamuziki Chameleone wa Uganda lazidi kuchukua sura mpya

Askari wa upelelezi akifanya vipimo eneo la tukio.(Picha kwa hisani ya newvision.co.ug).
Na.Mo Blog Team
Baba mzazi wa mtu aliyejulikana kama Robert Karamagi ambaye alifariki kutokana na majeraha ya kuungua kwa moto kwa kile kinachoaminika kuchomwa kwa makusudi ndani ya nyumba ya mwanamuziki Jose Chameleone wa Uganda ameibuka na kusema mtoto wake hakujilipua mwenyewe kama inavyodaiwa.
Karamagi aliyekuwa na umri wa miaka 27 alifariki katika hospitali ya Mulago saa chache baada ya kufikishwa hapo na kulazwa.
Matukio yaliyosababisha Karamagi aliyevamia nyumba ya msanii huyo kukumbwa na mkasa huo bado ni kitendawili huko mke wa Chameleone Bi. Daniella akisisitiza kuwa Karamagi alijitia moto mwenyewe alipotaka kujaribi kumchoma bibie huyo.

Askari wa jeshi la polisi Uganda wakifanya mahojiano na Jose Chameleone (wa pili kushoto) nje ya nyumba yake.(Picha kwa hisani ya newvision.co.ug).
Lakini baba wa mtu huyo Meja Benedict Kyamanywa amepingana na ripoti kuwa mwanawe alijichoma moto mwenyewe.
Amesisitiza kuwa mwanaye alifungwa kwa kamba na kuchomwa moto ndani ya makazi ya mwanamuziki huyo.
Ameongoza kuwa kabla mwanaye huyo hajakata roho alimuambia kuwa alifungwa kamba na kuchomwa na mafuta ya ndege.
Hata hivyo katika hatua nyingine Meja Kyamanywa ambaye ni daktari msaidizi wa Kakiri Barracks amesema kuwa mtoto wa alikuwa na matatizo ya akili, na kuwa kijiji kizima kilikuwa kinajua akiwemo Chameleone mwenyewe.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...