


Kiongozi
wa kundi la uasi la M23, Jean Marie Runiga amezungumza na Idhaa ya
Kiswahili ya Sauti ya Amerika Ijumaa katika mahojiano ya moja kwa moja
na kusema yeye ni mtumishi wa Mungu na kwamba ni askofu aliyeamua
kuunda kundi la waasi ili ‘kutetea haki za wanyonge’ katika Jamhuri ya
kidemokrasi ya Congo.
Bw.
Runiga amesema Mungu hapendi kuona binadamu wakitaabika na hivyo
aliona kheri kuanza juhudi kuwakomboa wakongomani ambao hawajui maisha
mengine ila taabu na mateso. Kiongozi huyo wa M23 amesema serikali ya
Kabila imeshindwa kuwahudumia raia wa Congo na kwamba wengi wanakufa
kila siku sio kwa sababu ya vita bali ukosefu wa huduma za kimsingi kama
vile chakula na matibabu.
Alisema DRC haina miundombinu, haina barabara, haina hospitali , wala shule za kutegemewa. Alisema wanawake wanazidi kubakwa yote haya akilaumu uongozi anaosema si halali wa serikali ya Rais Joseph Kabila. Bw. Runiga amesema mwishoni mwa wiki hii kundi lake na wawakilishi wa serikali ya DRC wanakutana Kampala, Uganda kuendela na juhudi mazungumzo ya kutafuta amani nchini Congo. Alisisitiza kuwa kundi lake linatoa nafasi ya amani kwanza, kwa ajili ya raia wa Congo.
Alisema DRC haina miundombinu, haina barabara, haina hospitali , wala shule za kutegemewa. Alisema wanawake wanazidi kubakwa yote haya akilaumu uongozi anaosema si halali wa serikali ya Rais Joseph Kabila. Bw. Runiga amesema mwishoni mwa wiki hii kundi lake na wawakilishi wa serikali ya DRC wanakutana Kampala, Uganda kuendela na juhudi mazungumzo ya kutafuta amani nchini Congo. Alisisitiza kuwa kundi lake linatoa nafasi ya amani kwanza, kwa ajili ya raia wa Congo.

No comments:
Post a Comment