ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Sunday, January 27, 2013

TAARIFA YA NDUGU ZITTO KABWE (MB) KUHUSU YANAYOENDELEAMTWARA NA MRADI WA BOMBA LA GESI



 
 
Zitto Kabwe 


ASILIASerikali iache kutafuta mchawi, iende Mtwara
Katika kipindi cha wiki nne sasa kumekuwa na maandamamo, malumbano na vurugukuhusu mradi wa kujenga bomba la kusafirisha gesi asilia kutoka Mtwara hadi Dar esSalaam. Mradi huu wa kutandaza bomba la urefu wa kilometa 542 ni mkubwa sanahapa nchini, na una thamani kubwa zaidi kuliko miradi mingine yote ya miundombinuiliyopata kutokea hapa nchini. Mradi huu utajengwa kwa mkopo wa dola zaKimarekani 1.2 bilioni kutoka Benki ya Exim ya China.Wananchi wa Mtwara kupitia maandamano ya tarehe 27 Desemba 2012 wametakakujua hatma ya maendeleo ya mikoa wa kusini kutokana na mradi huu wa bomba lagesi. Serikali imewajibu wananchi hawa kwa kuwaita wahaini, watu hatari na wasioelewa. Imefika mahali inapotosha madai yao kwamba hawataki gesi itoke Mtwara.Kimsingi Serikali haijajibu hoja yeyote ya msingi ya wananchi wa Mtwara kuhusumradi wa kusafirisha gesi. Badala yake imekuwa ikijaribu kupotosha madai ya watuwa Mtwara kupitia mikutano na vyombo vya habari.Tangu maandamano haya yatokee, na baadaye mikutano ya hadhara nahatimaye matukio ya kusikitisha ya kuharibu mali za watu, mauaji yawatu na majeruhi mbalimbli, Serikali na hasa Wizara yenye dhamana yamradi huu, imekuwa ikitoa matamko kwenye vyombo vya habari badala yakwenda Mtwara kuzungumza na wananchi, kusikiliza madai yao na kuonanamna ya kutekeleza madai hayo. Kutokana na Serikali kutofanya hivyo,kusikiliza na kuzungumza na wananchi wa Mtwara, vurugu mbaya sana zimeendeleamkoani humo.Mwezi uliopita, Desemba 2012, tatizo lilionekana kuwa ndogo na lenye kuhusianazaidi na ukosefu wa kushirikishwa kwa wananchi. Badala ya kushughulikiatatizo likiwa bado ndogo, Serikali imeona njia pekee ya kushughulikia suala hili nikutafuta mchawi na kwa wiki zote hizi imekuwa ikisemakuwa w
anasiasa namakampuni ya uwekezaji ya nje yanachochea mgogorohuu
.Leo hali iliyopo mkoani Mtwara inasikitisha sana, maana mali za wananchizinaharibiwa, nyumba zinachomwa moto na watu wanapoteza maisha. Tunalaanimatukio haya kwa nguvu zetu zote, maana kinachotokea Mtwara si Utanzania.Tusipowasikiliza wananchi na kutatua mgogoro huu kwa kuwashirikisha, hali itazidikuzorota wakati tukitupiana lawama.Hivi sasa serikali imeona njia pekee ya kushughulikia suala hili ni kutafuta mchawi nakwa wiki zote hizi
imekuwa ikisema kuwa wanasiasa na makampuni ya uwekezajiya nje yanachochea mgogoro huu
.Kwanza, Serikali imekuwa ikiaminisha umma kwanza suala hili limechukuliwakisiasa. Pili, Serikali imekuwa ikirudia kusema kuwa baadhi ya makampuni ya
 
uwekezaji nchini na mataifa ya Magharibi yamekuwa yakichochea wananchi waMtwara.Katika mwendelezo wa mtindo wa Serikali wa ‘
management by press conferences’
 jana Jumamosi Naibu Waziri wa Nishati na Madini ndugu George Simbachawenealiwaambia wahariri kwamba mimi Zitto Kabwe ninachochea wananchi wa Mtwara,ninatumiwa, na si mzalendo. Vile vile alitoa vielelezo kadhaa kuonyesha kuwa mradiwa kujenga bomba la gesi ni gharama sawasawa. Akasisitiza kwamba mimi nimwongo.Katika kipindi chote cha mgogoro wa Gesi Mtwara, sijafika Mtwara. Sijafanyamkutano wowote na waandishi zaidi ya kuandika mawazo yangu, kama Mtanzaniakuhusu suala hili.Nimeandika makala nne na zimechapishwa katika magazeti kadhaa hapa nchini nakwenye blogu yangu (http://zittokabwe.wordpress.com/).
Niliandika: 

 ni baadhi ya makala nilizoandika kuhusiana na suala la Mtwara. Sitaki kubishana na Naibu Waziri ama Kiongozi yeyote ya Serikali kwa sasa.Hatuwezi kuendelea kulumbana, kuzozana, kuzodoana na kurushiana manenowakati nchi yetu inaungua. Huu sio wakati wa kutafuta mchawi bali kutafutamajawabu ya changamoto zilizopo mbele yetu.Yanayotokea Mtwara ni fundisho kwetu kwa Taifa namna ya kukabili changamoto zautajiri wa rasilimali, ili kuweka mkakati, mambo haya yanayotokea Mtwara yasitokeetena Tanzania. Tutaweza kuzuia maafa haya iwapo tutaweka uwazi katika mikataba,tutashirikisha wananchi kwenye unyonyaji wa maliasili za nchi, na iwapo tutawekauwajibikaji.
Rais Kikwete Kikwete ana majibu; ayatoe sasa kwa wana Mtwara
Kwa mujibu wa Mpango Kabambe wa Umeme nchini (Power System Master Plan),kulikuwa na mradi wa kufua umeme MnaziBay, ambao Rais Jakaya Kikwete aliagizautekelezwe mara moja. Serikali ieleze umma kuhusu mradi huo wa kujenga kituo chakufua umeme 300MW MnaziBay Mtwara na kujenga msongo wa umeme wa 300KVmpaka Singida. Umeishia wapi? Ikumbukwe kuwa mnamo tarehe 12 Oktoba 2012,Rais Jakaya Kikwete alipokea ripoti ya ujenzi wa mradi huu kutoka makampuni yaChina National Machinery & Equipment Import & Export Corporation (CMEC) yaChina na Siemens ya Ujerumani, ambayo kwa pamoja yalitarajia kujenga kituokikubwa cha kuzalisha umeme kutokana na gesi katika eneo la Mnazi Bay, mjiniMtwara na pia kujenga njia ya kusafirisha umeme ya kilomita 1,100 kutoka Mtwarahadi Singida. Mradi huu ungegarimu dola za kimarekani milioni 684 na Rais aliagizautekelezwe haraka sana. Huu mradi uliishia wapi? Kwa nini Serikali ipo kimya
kuhusu mradi huu ambao ungejibu kabisa maswali ya watu wa Mtwara?
Taarifa yaIkulu kuhusu mradi huu imeambatanishwa hapa Tufanyeje?
Hapa tulipofikia ni lazima kwanza kabisa kusikia kilio cha wananchi wa Mtwaraikiwemo kuelewa madai yao. Swali kubwa kubwa la watu wa Mtwara na Kusini kwaujumla ni ‘tunanufaikaje’? Jibu la swali hili si ahadi za miradi bali ni vitendo. Hapandipo serikali inaposhindwa kushughulikia suala hili, kutoelewa madai ya wananchina kuyapotosha.Viongozi wa kisiasa wenye ushawishi kutoka pande zote, chamatawala na vyama vya upinzani, waende Mtwara kuzungumza na wananchi, lakiniwawasikilize kwanza.
1.Lazima viongozi tujenge utamaduni wa kusikiliza wananchi na si kuwahutubia tu. Wananchi wa Mtwara wana madai ambayo lazima viongozi tukae kitakokuwasikiliza kisha kufanya nao majadiliano ambayo yatatoa mwafaka. Raismstaafu,
Ndugu Benjamin Mkapa ameshatoa kauli kuhusu suala hili. Ni wakati mwafaka sasa kwa viogozi wengine kumuunga mkono kwakwenda Mtwara na kukaa na wananchi wa Wilaya zote za Mtwara,kusikiliza hoja zao na kuona namna ya kupata ufumbuzi wa suala hili.Wakati hatua hii inachukuliwa, wananchi waombwe kutulia na kuachavurugu za aina yeyote ile, na Serikali isimamishe mradi mpaka haposuluhu na wananchi itakapopatikana
.
2.Wakati juhudi hizo zinaendelea
Serikali iweke wazi mkataba wa ujenzi wabomba, kwani ni dhahiri gharama za mradi huu ni kubwa mno kulinganana uhalisia wa miradi ya namna hii duniani kote. Katika taarifa zote kwaumma Serikali imekuwa ikisema kwamba mradi utagharimu jumla yadola za kimarekani 1.2 bilioni, lakini katika taarifa ambayo Wizara yaNishati na Madini imesambaza jana kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini imesema mradi utagharimu dola za kimarekani milioni 875. Usiri katika mkataba huu unaashiria kwamba Serikali inaficha kitu.
Hivyo njiapekee ni kutaka mkataba uwe wazi kwa wananchi.
3.Wakati tunawataka wananchi wa Mtwara kuruhusu utulivu, ni vema Serikali ijiandae kutoa majawabu ya madai ya wananchi hao. Majawabu ya Serikali yajikite kueleza wananchi wa Mtwara wanafaidikaje na rasilimali ya gesi asiliakwa maendeleo yao. Wananchi wa Mtwara wanataka uwajibikaji wa Serikali kwenye utajiri wa nchi, na wamechoka na porojo za orodha ya miradi isiyotekelezwa
.Viongozi twendeni Mtwara kusikiliza wananchi wetu. Nchi inaungua na hatuwezi kuendelea kuzozana badala ya kuzima moto huu hatari kama vita vya MajiMaji. Miminakwenda Mtwara haraka na mara baada ya viongozi wangu wa chama kutoa ridhaa.
ZITTO KABWE
Mbunge, Kigoma Mjini (Chadema)Waziri Kivuli wa Fedha

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...