Wakati mjadala mkubwa wa kutengeneza
silaha za nyuklia ukiendelea duniani juu ya Iran, kuna maandalizi makubwa za
vita vya kuangamiza panya nchini humo.
Nchini Iran Idadi ya panya hao
wakubwa imekuwa kubwa kuliko idadi ya wananchi woe na wameleta kero kubwa kwa
binadamu.
Panya hao wenye uzito wa zaidi ya
paudi 11 wameshindikana kuuwawa baada ya kampeni ya kuwauwa kwa sumu kushindwa.
Hivyo serikali jijini Teheran imeunda vikosi 40 vya walenga shabaha mahiri
ambao kazi yao ni kuwavizia na kuwauwa panya kwa silaha za moto.
Walenga shabaha hao wanaotumia bunduki za rifles zenye mwanga wa infra-red wameshafanikiwa kuwauwa panya 2000 wiki iliyopita.
Walenga shabaha hao wanaotumia bunduki za rifles zenye mwanga wa infra-red wameshafanikiwa kuwauwa panya 2000 wiki iliyopita.
Katika jiji la Teheran lenye wakazi
zaidi ya milioni 12 inakadiriwa panya wake kuwa na idadi ya mara mbili ya
wakazi hao yaani milioni 24. Mamlaka za Miji mikubwa hasa Teheran zimeanza
rasmi vita hivyo ambavyo wanafikiri vitaweza kuzaa matunda ya kuwaangamiza
panya hao.
Vita vyetu vya kupambana na mbu
waenezao malaria ni vya iaka mingi. Tuna cha kujifunza kwa wenzetu?
kweli mdau inatisha panya kama mbwa sasa ningekua nimimi nisinge fuga mbwa watati kupanya wakubwa nawanafaa kulinda
ReplyDelete