ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Friday, March 8, 2013

Mtoto ashinda kiti cha Udiwani Kenya


Mr Kibiwott Munge, who won the Lembus Perkerra ward URP ticket, has had a good run in the election campaigns and is now hoping his maiden attempt in competitive politics will not be in vain. He is 19 years old.



 Mtoto wa miaka 19 ametengeneza historia kwa kuwa mtoto wa kwanza Kenya kuwa Diwani akiwa na umri wa miaka 19 tu.  Kibiwott Munge, ambaye amegombea  kupitia chama cha URP, ameshinda katika jimbo la  Lembus Perkera huko Baringo kwa kura 3,333 hivyo kumfanya aandike historia ya kuwa Mkenya wa kwanza mdogo zaidi kupata udiwani.
Kufuatia ushindi huu, watu mbalimbali wakiwemo wanafunzi wa Sekondari  aliyowahi kusoma iitwayo Tenges Boys High School, wanafunzi walishangilia kwa furaha kuu ushindi huu wa Kibiwott. 

“Huu ni ushindi kwa vijana na hii inaonyesha kwamba vijana wana uwezo mkubwa wa kuiongoza nchi" alisema Mheshimiwa Munge katika hotuba yake ya kukubali  matokeo hayo yaliyompa ushindi.

Hata hivyo, Mheshimiwa Munge amewashukuru wazazi wake kwa kumpa baraka zao na pia anamshukuru sana rafiki yake wa karibu Mr. Njoroge ambaye alimwazima  pikipiki yake ambayo  kijana huyu ndiyo aliyoitumia katika kampeni zake zote hadi kufanikiwa kuchaguliwa.

Mtoto huyu  anasema kwamba alipata uzoefu na nia ya kuwa kiongozi wa kisiasa hsa kwa kusoma gazeti  la Taifa Leo. Katika uwakilishi wake , Mheshimiwa Kibiwott Munge anaahidi kuwatetea vijana  ili waweze kuwa na maisha bora.

Hii ni changamoto kwa vijana wetu wa Tanzania badala ya kulalamika tu tuamue na sisi kuchukua hatua za kugombea maadam katiba inaruhusu  Mtanzania mwenye umri wa miaka 18 anaweza kugombea, basi tutumie fursa zinazojitokeza katika kugombea nafasi mbalimbali kwa nia ya kuleta mabadiliko ya kweli.
Uchaguzi kwa wenzetu wa Kenya ni kitu muhimu sana na tulishuhudia mwananchi mmoja akilia kwa uchungu sana baada ya jina lake kutoonekana katika karatasi ya kupigia kura. Alilia kwa uchungu kwa sababu kura yake moja tu ingeweza kuleta mabadiliko makubwa. 50%+1

Kwa hapa kwetu watu milioni 5 tu kupiga kura wakati wenye sifa za kupiga kura tunazidi milioni 20 ni vigumu kuleta mabadiliko tunayopigia kelele kila siku. Kura ndiyo msemaji au mkombozi wa mwisho wa matatizo yanayotuzunguka. Tusiwaache wachache watuamulie. Nafasi ya kuamua inapopatikana basi tuitumie kikamilifu.

Na mdau: Bahati

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...