ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Saturday, April 13, 2013

FREEMAN MBOWE AMKAANGA ZITO KABWE...ADAI KUWA LWAKATARE HATOFUKUZWA CHADEMA HATA KAMA NI GAIDI


Katika hali ya kushitua,Mh.Mbowe akiongea na wanachama wa chadema jana Ubungo plaza amemkaanga Zitto kabwe na kudai kuwa chadema haiko tayari kumtimua Lwakatare katika chama hata kama ni gaidi.... 

"Eti nashangaa kuna watu wanataka CHADEMA kimuache Lwakatare na kumsimamisha uongozi kwa uzushi uliopandikizwa na CCM, Hilo halitafanyika"- alisema Mbowe.
IKUMBUKWE siku chache zilizopita naibu katibu Mkuu wa CHADEMA Mh. Zitto Kabwe alitoa mapendekezo ya kuomba Mshitakiwa mkuu kwenye kesi ya Ugaidi ambaye ni Ndugu Lwakatare aliyekuwa mkuu wa usalama wa chadema awajibike kisiasa... 
Kuwajibika kisiasa ni pamoja na kuachia ngazi ya ukurugenzi wa usalama ili kupisha uchunguzi salama na kukiacha chama salama. 
Katika barua yake kwa chama chake,Zitto Kabwe alikitaka chama kijichunguze kuhusu shutuma hizi za ugaidi zinazokikabili huku Lwakatare akiwa nje ya ulingo wa viongozi waandamizi wa chadema.


Hata hivyo katika hali ya kustaabisha barua ya zitto ilivuja na kusambaa mitandaoni wakati Zitto Kabwe anadai kuwa ilikuwa ni barua ya siri kati yake na ofisi ya katibu mkuu wa chadema....
Kauli ya Mbowe leo hii kumkana zitto Kbwe mbele ya wanachama wa inaleta sura mbili ndani ya chama hicho cha upinzani:
Mosi:Barua ya mapendekezo ya Zitto ilivujishwa kwa maksudi kama njia ya kumpinga zitto....
Pili: Kauli ya Mbowe ya leo inamkingia kifua katibu mkuu kutowajibika kwa kuvujisha barua kwa sababu barua haikubebe ujumbe wenye maana kwa chama na Lwaktare 
Tatu: Madai ya UGAIDI dhidi ya Lwakatare na Chadema kwa ujumla ni ya kweli ,hivyo chama kinajukumu la kumlinda Lwakatare ili kuuficha ukweli usijulikana

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...