ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Wednesday, April 10, 2013

UFAFANUZI KUHUSU SERIKALI KUWAPATIA WANANCHI SEHEMU KUBWA YA ENEO LA PORI TENGEFU LA LOLIONDO




SONY DSCWAZIRIWIZARA YA MALIASILI NA UTALII Mhe. Balozi Khamis Kagasheki akitoa ufafanuzi kuhusu eneo la pori TENGEFU LA LOLIONDO Kwa waandishi wa habari leo ofisini kwake jijini Dar es salaam.
(PICHA NA PHILEMON SOLOMONWA FULLSHANGWE )
********
SERIKALI inasikitishwa na baadhi ya Asasi za kirai na vyombo vya habari vinavyopotosha ukweli kuhusu mgogoro wa ardhi katika eneo la Pori Tengefu la Loliondo.
Hayo yamebainishwa na Waziri wa Maliasili na Utalii,Balozi Khamis Kagasheki alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam.
Kagasheki amesema kuwa eneo la pori tengefu la Loliondo ni miliki halali ya serikali kwa mujibu wa sheria ya umilikaji ardhi tokea kabla na baada ya ukoloni.Historia inaonyesha kuwa mwaka 1902 utawala wa ujerumani walitunga sheria ya umiliki na matumizi ya ardhi ambapo ardhi ilibaki kuwa chini ya serikali,vivyo hivyo kwa utawala wa Waingereza mnamo mwaka 1923 na 1974 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akitoa ufafanuzi kuhusu mgogoro huo Kagasheki amesema kuwa kinachofanyika sasa ni Serikali kumega ardhi yake na kuwapatia wananchi na si kama inavyoripotiwa na vyombo vingi vya habari.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...