ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Tuesday, June 18, 2013

Flashback Ya Mwenyekiti Wenu; Mwalimu Alipotinga Dodoma 1996



6 0952f
Ndugu zangu,

Nakumbuka mwaka 1996 Julius Nyerere alipokuwa Msuluhishi wa Migogoro ya nchi za Maziwa Makuu ( Burundi) , Mwalimu alitinga Bungeni Dodoma kuwaapa taarifa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juu ya maendeleo ya kazi yake ya usuluhishi.

Mbunge mmoja alisimama na kutamka; "Mwalimu, kwa nini Tanzania isiingie kijeshi na kuzichukua hizi nchi za Burundi na Rwanda na kuwa sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania."

Je, kuna mjumbe mwenye kumbukumbu zaidi ya tukio lile la Dodoma? Mbunge yule aliitwa nani? Na je, ingelikuwa leo, ingewezekana kusimama Mbunge na kutoa ushauri kama huo?

Maggid,
Iringa.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...