ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI
Showing posts with label Siasa. Show all posts
Showing posts with label Siasa. Show all posts

Thursday, March 12, 2015

Nape: Dk. Slaa ni Muongo na Mzushi aliyebobea Kiasi cha Kuitwa Dokta .........Aanika Maovu yake yote Amtaka amrudie Mwenyezi Mungu Haraka



Tarehe 08/03/2015, Dr. Wilbroad Slaa Katibu Mkuu wa Chadema kupitia kwa mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema Ndugu Mabere Marando alitoa tuhuma kwa Serikali na kuwahusisha baadhi ya viongozi wa juu wa CCM kuwa wanapanga njama za kumdhuru Katibu Mkuu huyo wa Chadema.

Kimsingi tuhuma hizi ni za kipuuzi, lakini uongo huu usipojibiwa unaweza kugeuzwa kuwa ajenda na Chama hiki cha Chadema kwa kukosa ajenda zingine za maana. Hakuna asiyejua kuwa Chadema kwa sasa kinapumulia mashine, hivyo maneno na matendo yao kwa sasa lazima yalenge kujaribu kujinasua na balaa la kufa kwa chama chao.

Ni vizuri Watanzania wakakumbuka historia ya tuhuma lukuki zilizowahi kutolewana Katibu Mkuu huyu wa Chadema toka aanze siasa na ambazo zote zilikuja thibitika kuwa ni za uongo. Hapa nitawakumbusha baadhi.


Akiwa Singida katika kampeni za Urais za mwaka 2010,Dk. Slaa aliwatangazia wananchi mkutanoni kwamba kulikuwa kumekamatwa lori kubwa la mizigo (semi-trela) lililojazwa karatasi za kura za Urais zilizokuwa tayari amepigiwa kabisa mgombea Urais wa CCM, Dk.Jakaya Kikwete. Katika kuonyesha kwamba alikuwa na uhakika wajambo hilo, alisoma hadi namba za lori hilo na tela lake kutoka kwenye karatasi aliyokuwa ameshika mkononi, kisha akasema kuwa lori hilo lilikamatwa katika mji mdogo wa Tunduma, mkoa wa Mbeya wakati likiingia nchini kutoka Lusaka, Zambia.
Lakini baada ya polisi kuchukua hatua za haraka wakitumia namba za lori na tela lake alizokuwa amezisoma na kulikamata, kisha wakalipekua hadharani huku wananchi wakishuhudia palepale Tunduma, kilichokutwa ndani ya lori ilikuwa shehena ya vipodozi vya kina mama na sabuni za manukato.Baada ya siku chache huku akiwa amesahau yote, Dk.Slaa akatangaza tena kuwa mgombea Urais wa CCM, Rais Jakaya Kikwete alikesha katika hoteli ya Lakairo, Mwanza akiweka mikakati ya kuiba kura siku ya uchaguzi huo wa mwaka 2010 ili ashinde. Siku chache alisema kura zimeingizwa na zimeshapigwa, hapa amesahau anadai ndio kwanza mpango unapangwa.

Aliwataja watu wengine aliodai walikuwa pamoja na Rais Kikwete kuwa ni aliyekuwa Mbunge wa Igunga,Rostam Aziz na Mkurugenzi wa Hoteli hiyo iliyopo katika jiji la Mwanza, Lameck Airo.

Lakini wakati Dk. Slaa akisema uongo huo,Rais Kikwete siku nzima na usiku wake wote alikuwa Mtwara akiendelea na kampeni zake za Urais.

Hata Rostam Aziz naye kwa siku hiyo pamoja na usiku wake wote alikuwa Igunga akiendelea na kampeni zake za Ubunge, na pia hata Airo naye siku nzima na usiku wote huo alikuwa jimboni kwake Rorya akifanya kampeni zake za kugombea Ubunge.

Baada ya kushindwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, Dk. Slaa aliwaambia waandishi wa habari kwamba alikuwa na ushahidi wa matokeo ya Urais ya kituo kwa kituo ya nchi nzima yakionyesha kuwa alishinda.

Akasema, chama chake kingeyasoma hadharani na kuwakabidhi waandishi wa habari ili wananchi waujue ukweli kuwa alidhulumiwa ushindi wake, kazi iliyofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi na haki yake akapewa aliyekuwa mgombea Urais wa CCM, Jakaya Kikwete.

Lakini kwa vile alikuwa akiwatangazia uongo wananchi, Dk. Slaa hadi leo hajawahi kuyasoma matokeo hayo ya kughushi, badala yake alipowaita tena waandishi wa habari akatangaza kuwa Tanzania isingetawalika mpaka arudishiwe haki yake. Hapo ndipo ghasia zikiwemo za mauaji za Chadema zilipoanza hadi leo.
Januari, 2011 aliwaambia waandishi wa habari kwamba alikuwa na mkanda unaothibitisha kuwa mauaji ya Januari 5, mwaka huo yaliyofanyika katika jiji la Arusha kutokana na maandamano ya vurugu ya wafuasi wa Chadema yalifanywa kwa makusudi na polisi, na kwamba wafuasi wake hawakufanya fujo wala vurugu zozote.

Alisema mkanda huo angeuonyesha mbele ya waandishi wa habari ndani ya siku tatu au mbili baada ya Polisi Makao Makuu,kuonyesha unaothibitisha kwamba wafuasi wa Chadema walifanya vurugu ikiwemo kutaka kuvamia Jengo la Makao Makuu ya Polisi la Mkoa na kupora silaha zilizokuwa humo, wawafungulie wahalifu waliokuwa ndani na kulichoma moto jengo lenyewe.

Lakini tokea kipindi hicho hadi sasa ikiwa tayari imeshapita miaka minne, Dk. Slaa siyo tu ameshindwa kuuonyesha mkanda huo “ndani ya siku tatu ama mbili” alizokuwa ameahidi, bali amethibitisha kwamba alichosema kwa Watanzania ulikuwa ni uongo na uzushi.
Mwaka 2011, Dr. Slaa alikwenda mbali kwa kuzusha kwenye mkutano wa hadhara kuwa aliyekua Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga wakati huu Brig. Gen. mstaafu Yohana Balele amefariki dunia.

Akajaribu kuwaaminisha wananchi pale kuwa ni kweli, baadae ikagundulika kuwa Mkuu huyo wa Mkoa ni mzima na wala haumwi. Haikujulikana mara moja sababu za Dr. Slaa kumzushia kifo Mkuu huyo wa Mkoa.
Julai 2012, Dr. Slaa na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika walizusha kwamba wanafuatiliwa na baadhi ya Maafisa wa Idara ya Usalama wa Taifa ili wauawe, lakini walipotakiwa kupeleka ushahidi wao katika vyombo vya dola ili kusudi watuhumiwa wachunguzwe na hatimaye wakamatwe na kuruhusu Sheria ichukue mkondo wake, wote waligoma na kudai hawapo tayari kushirikiana na Jeshi la Polisi.

Waliendelea na msimamo huo hata pale Dk. Slaa alipolazimishwa kwenda Makao Makuu ya Jeshi la Polisi na kuhojiwa, lakini akashindwa kutoa uthibitisho wake mwenyewe wala wa Mnyika kwa sababu walidai suala hilo limezungumzwa katika kikao cha Kamati Kuu ya Chadema.
Mwaka 2012, Dr. Slaa akiwa ziarani Ifakara wilayani Kilombero mkoa wa Morogoro, alidai kuwa CCM imeingiza silaha kutoka nje ya nchi kontena zima, ili zitumike kuwadhuru viongozi wa Chadema, jambo ambalo hata hivyo hadi leo ameshindwa kulitolea uthibitisho wala kielelezo chochote.

Wanaomfahamu vizuri endapo ingekuwa kweli angeita waandishi wa habari, akatoa ushahidi wake na kuwakabidhi ili wautumie kuandika madai hayo, lakini kwa sababu ulikuwa ni uongo ndiyo maana hakutoa karatasi yoyote hadi leo.
Juzi bila aibu anaibuka na tuhuma zingine za eti kutaka kuuawa. Kupanga kumdhuru Dr. Slaa, ili CCM ipate nini kwa kudhurika kwake? Kwa umri wake, afya yake na kadhalika, kwa nini CCM ipange kumdhuru mzee huyu? Huu ni mwendelezo wa tabia yake ya kuzusha mambo ya uongo kila anapoona anachuja kisiasa. Ni busara kwa umri wake akatumia muda wake mwingi KUMRUDIA MWENYEZI MUNGU.



Lakini hata mtu aliyetumika kuufikisha uongo huo kwa umma, naye ana historia ya kuzusha mambo na kusema hata asiyoyaamini.

Marando aliwahi kuitisha kikao na waandishi wa habari na kudai Katibu wa Itikadi na Uenezi alifaidika na pesa za EPA, alipobanwa na mteja wake aliyekuwa akimtetea mahakamani kwa kesi hiyo hiyo ya EPA, akaruka yale matamshi yake kwa maandishi na kudai ilikuwa ni shinikizo la Chama chake kusoma yale maneno lakini hata yeye hayaamini.

Lakini ni Marando huyu huyu ambaye akipanda kwenye majukwaa ya siasa anadai swala la EPA ni ufisadi mkubwa sana kwa nchi na akishuka tu jukwaani, anakimbia mahakamani kwenda kuwatetea watuhumiwa hao hao wa EPA aliowaita majukwaani mafisadi wa EPA. Mzee huyu naye ni MNAFIKI.

Hebu tujiulize, ni lini Mabere Marando aliacha rasmi kazi yake ya awali ya ukachero mpaka aaminike leo kufanya kazi afanyayo? Nani alimtumia kujaribu kusambaratisha chama cha NCCR-Mageuzi miaka ya mwanzo ya mfumo wa vyama vingi nchini? Hivi ni kweli Marando ni wa kuaminiwa leo?

Natoa wito kwa Watanzania bila kuingilia utaratibu wa Sheria na vyombo vya Serikali kufuatilia uongo huu mpya, Watanzania nawaomba wampuuze na kupuuza uongo huu. Usitupotezee muda, tuendelee na mambo ya msingi ya kujenga nchi yetu.

Nimshauri pia BABU yangu Dr. Slaa, kwa umri wake, wenzake wakifikisha umri huu wa uzee wanatumia muda wao kumrejea Mwenyezi Mungu badala ya yeye kuendelea kutunga uongo na uzushi kila kukicha. Namwomba mwenyezi Mungu amuwezeshe kuiona busara hiyo.

Imetolewana:-


NapeMoses Nnauye,

KATIBUWA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,
ITIKADINA UENEZI10/03/2015

Tuesday, January 27, 2015

BREEKING NEWS, MABOMU YATAWALA MBAGALA, PROFESA LIPUMBA AKAMATWA, NI MAANDAMO YA CUF


HABARI zilizotufikia mda huu zinasema Jeshi la Polisi Mkoani Dar es Salaam limetumia nguvu kwa  kurusha mabomu ya machozi ili kuwatawanya wananchama cha Wananchi CUF waliokuwa kwenye maandamo wilaya ya Temeke .
Na kufanikiwa kuwatia nguvuni viongozi waandamizi wa chama cha Wananchi CUF,wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Profesa Ibrahimu Lipumba,huku wananchi wa maeneo hayo wakiishi kwa hofu kubwa sana.
Akithibitisha kukamatwa viongozi hao pamoja na kuvunjwa kwa maandamano .Afisa Habari wa chama cha Cuf ,Bwana Silas  alipoongea na mtandao huu mda huu ambapo amesema waalianza maandamano ya Amani katika Viwanja vya temeke na kwenda mbagala , ambapo maandamano hayo yaliokuwa na lengo la kumbukumbu ya mauaji ya wanachama wao yaliofanyika  TAREHE 26 januari mwaka  2001 huko Zanzibari na Tanzania Bara,
        Bwana Silas alisema wakati wapo kwenye maandamo hayo walipofika maeneo ya Mtongani iliyopo wilaya ya Temeke ndipo Jeshi la polisi likafika na kurusha mabomu na kuwapiga wanachama wa chama hicho na kufanikiwa kuwakamata viongozi wa chama hicho,na kuwapeleke kituo kikuu cha polisi.kwa madai maandamano hayo hayana ruhusa.

Tuesday, June 18, 2013

Flashback Ya Mwenyekiti Wenu; Mwalimu Alipotinga Dodoma 1996



6 0952f
Ndugu zangu,

Nakumbuka mwaka 1996 Julius Nyerere alipokuwa Msuluhishi wa Migogoro ya nchi za Maziwa Makuu ( Burundi) , Mwalimu alitinga Bungeni Dodoma kuwaapa taarifa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juu ya maendeleo ya kazi yake ya usuluhishi.

Mbunge mmoja alisimama na kutamka; "Mwalimu, kwa nini Tanzania isiingie kijeshi na kuzichukua hizi nchi za Burundi na Rwanda na kuwa sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania."

Je, kuna mjumbe mwenye kumbukumbu zaidi ya tukio lile la Dodoma? Mbunge yule aliitwa nani? Na je, ingelikuwa leo, ingewezekana kusimama Mbunge na kutoa ushauri kama huo?

Maggid,
Iringa.

CCM yaishutumu Chadema kuwa ndio wanaohusika na mlipuko Arusha.


Sunday, June 16, 2013

TAMKO RASMI LA CHADEMA KWA WANANCHI JUU YA KINACHOENDELEA KWENYE CHAGUZI NDOGO ZA MARUDIO KWA KATA MBALIMBALI NCHINI



Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinatoa taarifa za Hujuma zinazoendelea katika chaguzi za marudio kwa kata mbalimbali hapa nchini.
Kwa masikitiko makubwa CHADEMA kinatoa taarifa ya matukio ya kusikitisha yanayoendelea katika chaguzi hizi,kama ifuatavyo;

1. KATA YA IYELA,MBEYA.

Katika kata hii Gari la Chama Cha Mapinduzi lenye Usajili namba T 704 BEU,likiwa na watu wawili wanaotambulika kwa majina ya Moris na Nosy,waliwateka vijana wa CHADEMA na mmoja wao kuchomwa kisu,aliechomwa kisu anaitwa Meshack Bernard.Vijana wa CCM waliokamatwa wameachiwa huru na jeshi la polisi na sasa wanatumia gari nyingine yenye rangi nyekundu Toyata Surf namba T-173 ANE,wakiendelea kufanya vitendo hivo viovu.

Na katika kituo cha kupigia kura cha SIDO ,vituo 3 vimelundikwa sehemu moja na eneo hilo kuna Karakana ambayo inawafanya watu kuingia na kutoka kinyume na sheria za uchaguzi.

2. KATA YA MBALAMAZIWA ,MUFINDI KASKAZINI.
Watu sita wamepigwa kwa marungu na visu na kuumizwa vibaya muda huu.Idadi ya vitisho katika kata hii ni kubwa mno hali iliyopelekea idadi ndogo ya watu kujitokeza kupiga kura.

4. NYAMPU LUKANO, SENGEREMA 

Viongozi na makada wa CCM waligawa mapanga kwa vijana wao na kukata watu.Vijana 3 wa CHADEMA wamechomwa kisu na kujeruhiwa vibaya sana.

5:KATA YA MINEPA,MOROGORO.

Tukio lililotokea huko ni kuchomwa moto PIKIPIKI mali ya Chama(M4C) na vijana wa CCM(greenguard). Vile vile Katibu wa Chama wilaya ndugu Lucas Daniel amepigwa na kuumizwa na mwenzake amekatwa vidole.

3.KATA YA MANCHIRA,SERENGETI-MARA
Tumepokea taarifa kuwa Mkuu wa Wilaya kujihusisha na vitendo vya utoaji rushwa kwa wapiga kura,kwa lengo la kuwezesha CCM kushinda. Vijana wetu ni mashuhuda wa tukio hilo na wako tayari kutoa ushahidi juu ya hili piai wameshuhudia vijana wa CCM wakiwa na Bastola na baadhi yao kukamatwa na vijana wa CHADEMA na kupelekwa polisi

Hali kadhalika Jeshi la Polisi limekamata vijana wetu kuanzia jana jioni hadi leo hii na wamekuwa wakitumia mabomu na hivyo kuwajeruhi.Kuna vijana ambao wametekwa na hawajulikani walipo na majina yao na wanakotoka ni kama ifuatavyo
-Barena Maro-Bwitengi
-Samson Ogao-Rwamchanga
-Adam Samson-Bwitengi
-Emmanuel Eliya-Bwitengi
-Onyango Otaro-Miseke
-Manginare Samson-Miseke
-Elija Wilson-Miseke
-Banage Nanai-Rwamchanga
-Matororo saina-Rwamchanga
-Pikipiki Simba-Rwamchanga
John Oninga-Rwamchanga

Na baadhi ya gari zifuatazo zilikua zikishiriki opereshani ya kuwateka wafuasi wa CHADEMA magari hayo ni yenye namba zifuatazo za usajili T286 BFB, T545BFE zote Landcruiser za CCM na T352 AHD.
Diwani wa CHADEMA kata ya MUGUMU Mh.Marwa Waryoba amekamatwa na polisi yupo kituoni ili kumyima fursa ya kukugua zoezi la upigaji kura kama sheria inavyomtaka.

3. KATA YA MIANZINI,DAR ES SALAAM.
Tukio lililotokea huko ni kutekwa kwa wanachama na kiongozi wa Chama. Watu hawa walitekwa na kufungwa vitambaa vyeusi machoni,kisha kupigwa na kuumizwa vibaya. Mmoja kati ya vijana hao ni Katibu wa Vijana CHADEMA tawi la machinjioni anaeitwa Julius Vedastua na mpaka sasa yuko hospital.
Tukio lingine linaloendelea katika kata hii ni vitendo vya Rushwa,makada wa CCM wamekuwa wakivuta watu kutoka kwenye mistari na kuwapatia pesa.
Hali kadhalika kwa baadhi ya maeneo katika kata hii ni kuwa na wasimamizi wengi katika kituo kimoja,na wasimamizi hao wamekuwa wakiwaongoza watu kupiga kura mpaka kwenye ile sehemu ya kupigia kura na kuwapa maelezo juu ya nani wa kumchagua,kitendo ambacho ni kinyume na Sheria.

KATA YA STESHENI, NACHINGEA,LINDI.
Taarifa tulizonazo zinasema kuwa Magari ya CCM yamekuwa yakisomba wapiga kura na kati ya magari yanayotumika ni gari lenye usajili namba T670 DEU.

KATA YA DONGOBESH,MANYARA.
Katika kata hiyo,makada wa CCM wanawavamia katika vilabu vya pombe na kuwanunulia wananchi pombe kama hongo ya kutaka kupigiwa kura,na baada ya kuwanunulia pombe wamekuwa wakiwasomba kwa magari na kuwapeleka katika vituo vyao vya kupigia kura,kitendo hichi ambacho ni kinyume na sheria.

KATA YA GENGE,TANGA.
Matukio yaliyotokea huko ni vijana wa CCM kuwakamata vijana wetu wa Red Brigade na kuwapiga na kuwaumiza. Tukio hili limesharipotiwa polisi.

KATA YA MAKUYUNI,ARUSHA.
Vijana wa Kimasai ambao wamekodiwa na Chama cha Mapinduzi wamekuwa wakivamia wanachama na viongozi wetu na kuwapiga,katika kata hii ndio tukio la kumpiga na kumjeruhi Mh Mbunge Joshua Nasari limefanyika.

Aidha kuhusu mauaji ya Arusha Mwenyekiti wa Chama Taifa,Mh Freeman Mbowe ameshatoa


msimamo wa chama juu ya tukio hilo.


Imetolewa na :

Erasto Tumbo(Afisa Mwandamizi Uenezi)
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...