ADV

ADV

ADVERTISEMENT CORNER

HUDUMA YA KUKATA TICKET ZA NDEGE ONLINE


SOMA HABARI

SOMA HABARI

Tuesday, June 11, 2013

MADAKTARI WA MISRI KUTOA TIBA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI


Dk.-Hussein-Mwinyi 
NA MAGRETH     KINABO – MAELEZO
JUMLA  ya madaktari  sita na wataalamu wawili ,mmoja wa  teknolojia na mwingine wa utawala  kutoka  Misri  wamewasili nchini kwa ajili ya kutoa huduma ya upasuaji wa tundu ndogo kwenye Hospitali ya Taifa ya   Muhimbili(MNH) jijini Dare es Salaam.
Kauli hiyo imetolewa leo  na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein Mwinyi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ujio wa madaktari hao .
“Madaktari  hawa watasaidia kutoa  kutoa tiba na kuwafundisha madaktari wetu utaalamu huu, hivyo ujio wao utasaidia kupunguza gharama  za matibabu kwa wagonjwa wanaotakiwa kwenda nje ya nchi,” alisema Dk. Mwinyi.
Aliongeza kuwa  madakatari hao watakuwepo katika  hospitali hiyo kuanzia Juni 10 hadi 15, mwaka huu kwa ajili ya kutoa huduma hizo.
Dk. Mwinyi  aliushukuru ujio huo kwa kuwa utasaidia kubadilishana uzoefu na teknolojia na kuboresha  afya  ya Watanzania.
Kwa  upande wake, Balozi wa   Misri  nchini Tanzania, Hossam Omar  alisema ujio wa madaktari hao    ni kuendeleza ushirikiano baina ya nchi hizo mbili katika sekta hiyo, ambapo watauendeleza katika maeneo mengine ya sekta hiyo na nyingine.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...